DC Ubungo sasa Mkurugenzi mpya Tanesco
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Mwandishi Wetu,daimatzanews@gmail.com
Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Dar es Salaam Lazaro Jacob Twange kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
![]() |
Rais Samia Suluhu Hassan |
Uteuzi wa Twange umetangazwa Mei 7,2025 kupitia taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusiluka, iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga.
Twange aliyewahi kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),anachukua nafasi ya Mhandisi Nyamo-Hanga ambaye alifariki dunia kwa ajali ya gari.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni