Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2025

Ziara ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Anlex ya Dar es Salaam Bungeni mjini Dodoma

Picha
 Picha tofauti za wanafunzi wa Shule ya Msingi Anlex ya jijini Dar es Salaam Bungeni mjini Dodoma Mei 26 mwaka huu ( Picha na Mpiga picha Wetu).

Wafanyabiashara Kariakoo wapewa siku 14 kufungua barabara

Picha
 Na Hellen NGOROMERA, daimatznews@gmail,com MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ametoa wiki mbili kwa wafanyabiashara ndogo ndogo katika Soko la Kariakoo, kufungua barabara walizofunga kwa kuweka biashara zao. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila Chalamila amesema hayo Mei 28, 2025 jijini Dar es Salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Soko la Kariakoo. “Wafanyabiashara waliofunga barabara kwa kuweka meza na kuzuia uingiaji wa magari makubwa kwa ajili ya kuingiza biashara mbalimbali ndani ya soko. “Natoa rai kwao uongozi wa wafanyabiashara ndogo ndogo waanze kufungua biashara hizo ili mwisho wa siku soko litakapofunguliwa kusiwe na hitilafu ya aina yoyote kuhusu kuingia au kutoka kwa kutumia njia za sokoni hapo,” amesema RC Chalamila  akiongeza: "Wafanyabiashara hao wataniuliza watakwenda wapi? Katika soko jipya linalojengwa, wameratibu namna ya wafanyabiashara wote kukaa wakiwemo wafanyabishara ndogo ndogo kwa kuwek...

Waziri Jafo kufungua maonesho ya ‘Tanzania Dental Expo’ Dar kesho

Picha
Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Viwanda na Biashara,Dk.Selemani Jafo, anarajiwa kufungua maonesho ya huduma ya kinywa na meno  ‘Tanzania Dental Expo’ yatakayofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam kwa siku mbili kuanzia kesho Ijumaa Mei 30,2025. Mkurugenzi wa Tanzania Dental Expo Dk. Ambege Jack Mwakatobe. Maonesho hayo ya kihistoria yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  na Tanzania Dental Expo, pamoja na mambo mengine yawaleta pamoja wataalamu wa afya ya kinywa na meno kutoka ndani na nje ya Tanzania na maandalizi yamekamilika. "Kutakuwa na hudima  ya vipimo na ushauri bure wa kitaalamu kwa watu wenye matatizo ya afya ya kinywa na meno kutoka kwa wataalamu wabobevu. Lakini pia, kutakuwa na maonesho ya vifaa tiba vya kisasa vinavyotumika katika kutoa huduma na kuwawezesha watoa huduma wa ndani na nje kubadilishana uzoefu katika kuboresha sekta hiyo," amesema  Mkurugenzi wa Tanzania...

Rais ampeleka Ngorongoro Badru wa PSSSF, Dk. Doriye mhh..

Picha
 -Dk.Nyansaho bosi mpya PSSSF Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Rais Samia Suluhu Hassan,pichani chini ametengua uteuzi wa Dk. Elirehema Joshua Doriye aliyekuwa Kamishna wa Uhifadhi katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), huku akimteua Abdul-Razak Badru kushika nafasi hiyo. Kabla ya uteuzi huo,Badru alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), ambapo Rais Samia amemteua Dk. Rhimo Simeon Nyansaho kuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, awali alikuwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara katika Benki ya Azania.                            Dk. Nyansaho                                                 Abul- Razak Badru Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais – Ikul...

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Picha
  - Aichagua JKCI kupata huduma za kibingwa  - Burkina Faso yasaini makubaliano na JKCI  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais wa Burkina Faso,Kapteni Ibrahim Traore amefuata huduma bora za afya zinazotolewa nchini, hasa za magonjwa ya moyo. Rais wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traore Ndivyo unavyoweza kueleza, baada kiongozi huyo maarufu duniani,kutuma mwakilishi wake wa masuala ya afya Burkina Faso nchini kuzungumza na kutiliana saini hati ya makubaliano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), katika kutoa huduma bobezi ya matibabu ya  magonjwa ya moyo. Kwa mujibu wa JKCI, hati hizo zimesainiwa kati ya  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dk. Peter Kisenge na Mshauri wa Rais wa Burkina Faso na Mratibu wa Kitaifa wa Mpango wa Afya wa Rais, Drissa Traore, jana jijini Dar es Salaam. Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo, Dk. Kisenge amesema makubaliano hayo yataimarisha utoaji wa  huduma za matibab...

Masasi sasa kumekucha, NHC yaipa sura mpya

Picha
  - Yajenga jengo la Sh2.7 bilioni, kukamilika Septemba - Unaijua Jida? Sasa nenda Masasi Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Masasi kumekucha, ‘Jogoo’, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), limewika na kwa lugha ya wenyeji unaweza kusema ‘Masasi Kuchele’. Ndivyo unavyoweza kuielezea Mei 18,2025 siku ambayo historia mpya imeandikwa na NHC katika Mji wa Masasi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Mkoa wa Mtwara. Historia hiyo mpya iliyoandikwa ni kuzinduliwa ujenzi wa jengo jipya la Kituo cha Biashara, Masasi Commercial Complex kwa kuwekwa Jiwe la Msingi, huku aliyetimiza jukumu hilo akiwa pia kiongozi wa kihistoria kitaifa. Hakika hakuna wa kupinga kuwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2025, Ismail Ali Ussi kwani ni aghalab kiongozi wa mbio hizo kujirudia. Kuzinduliwa kwa Masasi Commercial Complex jengo ambalo ni la kisasa zaidi Masasi, wilaya inayobeba sehemu muhimu ya historia ya Tanzania, ikikumbukwa kuwa Rais wa Awamu ya Tatu, hayati Benjamin Mkapa alizaliwa w...

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMKARIBISHA RAIS WA NAMIBIA IKULU DAR

Picha
Picha mbalimbali zikionesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alivyomkaribisha Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah Ikulu muda mfupi baada ya kuwasili nchini kwa ziara rasmi, leo Mei 20, 2025.

Nafasi 2,000 za ajira Serikalini hizi hapa

Picha
-CAG azitambua taasisi yenye uhitaji -Ni taasisi 39 zimo balozi, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Wakati wimbi la vijana kukosa ajira likishuhudiwa na kupigiwa kelele na makundi mbalimbali ya kijamii nchini, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, imebainisha kuwepo kwa nafasi za kazi zilizo wazi zaidi ya 2,000 katika taasisi mbalimbali za Serikali na umma. Ripoti hiyo Kuu ya Mwaka ya Ukaguzi wa Serikali Kuu kwa mwaka 2023/24, iliyowasilishwa bungeni na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG), Charles Kichere hivi karibuni pichani juu, imezitaja taasisi 39 zenye upungufu wa watumishi wa taaluma mbalimbali, baadhi zikiwa ofisi za ubalozi wa Tanzania nje ya nchi, Jeshi la Polisi, Hospitali za Rufaa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. “Watumishi wanaohitajika kwenye taasisi hizo jumla ni 4490, waliopo ni 2288 na upungufu ni watumishi 2202,” imebainisha ripoti hiyo ya CAG.   Kwa mijibu wa CAG taa...

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi

Picha
Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Tanzania imepiga hatua isiyosahaulika katika historia ya maendeleo yake, baada ya kikosi cha wawekezaji wa ngazi ya juu kutoka Ufalme wa Oman, kufanya ziara nchini na kukutana na uongozi wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), wakifungua fursa kubwa za mabadiliko makubwa katika sekta ya nyumba na maendeleo ya miji nchini. Ujumbe wa Wawekezaji kutoka Oman(kulia) ukiwa katika mkutano na uongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), (kushoto), makao makuu ya shirika hilo jijini Dar es Salaam Mei 20,2024. Ujumbe huo uliongozwa na Balozi wa Oman nchini Tanzania, Saud Al Shidha, ulikuwa na malengo kadhaa ya kukuza ushirikiano wa kiuchumi ikiwamo kuanzisha mabadiliko ya kimkakati, yatakayochochea ukuaji wa sekta ya makazi kwa njia ya ubia wa kimataifa. Katika kikao cha kihistoria kilichofanyika Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) – Kambarage House, ujumbe wa Oman ulipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, pamoja na viongozi waandamizi w...

Mwenge wa Uhuru wazindua jengo la kisasa la NHC Masasi

Picha
 -Ni la Sh bilioni 2.7 -NHC yapongezwa Mwandishi Wetu. daimatznews@gmail.com Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka 2025, Ismail Ali Ussi amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kwa kazi kubwa ya kutekeleza kwa vitendo ndoto za kuboresha huduma za jamii na wafanyabiashara nchini kupitia sekta ya nyumba, kwa kujenga majengo bora ya kisasa yanayokidhi na kuchochea kasi ya maendeleo na uchumi wa taifa. Kiongozi wa Mwenge Kitaifa mwaka 2025, Ismail Ali Ussi (Kulia), akizungumza leo Mei 18, 2-25, baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi Kituo cha Biashara, Masasi Commercial Complex kinachojengwana Shirika la Nyumba la Taifa(NHC), wilayani Masasi, Mkoa wa Mtwara. Ametoa pongezi hizo leo Mei 18,2025 mjini Masasi mkoani Mtwara, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la kituo cha biashara lijulikanalo kwa jina la Masasi Commercial Complex linalojengwa na NHC. Jengo hilo litakapokamilika litakuwa na thamani ya Shilingi bilioni 2.7, huku shirika hilo likiahidi kukamil...

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi yatangaza majimbo mapya 8 ya uchaguzi

Picha
- Dar sasa majimbo 8, mapya ni  Chamazi na Kivule -Wabunge kuongezeka Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, (INEC), imetangaza majimbo mapya nane ya uchaguzi katika uchaguzi mkuu ujao wa madiwani, wabunge na Rais, huku ikibadili majina ya majimbo tisa. Mwenyekiti wa INEC,Jaji wa Rufaa, J acob's C Mo Mwambegele   Katika mabadiliko hayo yaliyotangazwa leo na tume hiyo, mikoa ya Dar es Salaam na Geita imefadiika zaidi kwa kuongezewa majimbo mawili kila mmoja, ambapo Dar es Salaam majimbo mapya ni Chamazi na Kivule, huku Geita mapya yakiwa Katoro na Chato Kusini.  Kufuatia mabadiliko hayo, Dar sasa itakuwa na majimbo nane kutoka sita ya awali ambayo ni Ilala, Kinononi, Mbagala, Temeke, Ubungo na Kibamba, Chamazi (jipya) na Kivule (jipya). Geita pia itakuwa na majimbo nane ambayo ni Chato Kusini, Chato Kaskazini, Katoro, Butundwe, Busanda, Nyang’wale, Mbogwe na Bukombe. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa, J acob's C Mo M...

Habemus Papam; Moshi mweupe watokea Vatican tumepata Papa

Picha
-Ni Kardinali Robert Prevost wa Chicago Marekani -Sasa ni Papa Leo wa XIV Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Habemus Papam;Ndiyo maneno yanayotamkwa kwa kilatini, kutangazia ulimwengu kwamba Papa amepatikana.  Papa Leo wa XIV, akisalimia umati wa waamini waliofirika viwanja vya St.Peters Vatican, mara baada ya kutangazwa kuwa kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki duniani.  Ndivyo ilivyotokea leo, historia mpya imeandikwa kwa Kanisa Katoliki,ambapo kwa mara ya kwanza Mmarekani amechaguliwa kuwa Papa.  Leo Alhamisi Mei 08, Baraza la Makardinali lililokuwa likikutana ndani ya Kanisa la Sistine kwa katika mkutano wa siri wa uchaguzi wa Papa limemchagua Kardinali Robert Prevost, mzaliwa wa Chicago, kuliongoza Kanisa Katoliki.duniani. Kardinali Robert Prevost amekubali wadhifa wake mpya kuwa Askofu wa Roma na kiongozi wa kiroho wa Wakatoliki zaidi ya bilioni 1.4 duniani, huku akichagua jina la Papa Leo wa XIV. Kwa siku ya pili leo kuanzia jana Mei 7,2025, makardinali 133 wa Kanis...