Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2025

Kaka ambwaga dada kesi ya mirathi Tabora

Picha
-Ni ya nyumba ya Zena Jalalkhan - Mahakama yasema Mleta Maombi amedai nyumba ya Zainab si Zena Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAHAKAMA ya Wilaya ya Nzega imetupilia mbali maombi ya Salma Kassam aliyetaka mahakama hiyo ichunguze usahihi na uhalali wa kaka yake kuteuliwa kusimamia mirathi ya mama yao Zena Jalalkhan. Jengo la Mahakama,wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora.  Uamuzi wa Mahakama hiyo umetolewa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi N. Mkadam, baada ya kupitia maombi na majibu ya Mjibu Maombi. Katika shauri hilo, Mleta Maombi ni Salma Kassam na Mjibu Maombi ni kaka yake Karim Samji.  Mleta Maombi aliwasilisha maombi yake chini ya hati ya dharura na kuambatanisha  hati ya kiapo. Katika maombi yake, Salma alikuwa na hoja tatu, ikiwamo kuiomba mahakama uufanyie marejeo mwenendo wa shauri la mirathi katika Mahakama ya Mwanzo Nyasa na hukumu iliyotolewa kwenye shauri hilo la mirathi namba 23 na 35 ya mwaka 2023. Aliomba mahakama ichunguze usahihi na uhalali wa Mjibu Maombi...

Kamati ya Bunge yasifu kazi ya NHC

Picha
  Kamati ya Bunge yasifu kazi ya NHC  -Wizara ya Madini kuanza kazi Mtumba Mei 15 Mwandishi Wetu Daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba laTaifa(NHC), limeendelea kung’ara katika utekelezaji miradi mikubwa ya ujenzi likipongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, huku Wazara ya Madini ikitangaza itaanza utoaji huduma kutoka ofisi yake mpya katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma ifikapo Mei. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imetoa pongezi hizo katika ziara yake kwenye Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma kukagua miradi ya ujenzi wa majengo ya ofisi za Wizara ya Madini na ule wa Nishati, ambapo Waziri wa Madini,Anthony Mavunde ameutangazia umma kuwa watumishi wote wa wizara akiwamo yeye wataanza kuhudumia wananchi kutoka kwenye jengo hilo jipya  kuanzia Mei 15, 2025.   Kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake, Dk. Mathayo David Mathayo, ilifanya ziara pia katika Jengo la Wizara ya Nishati.  Dk.Mathayo ameeleza kuridhishwa kwa kamati na kiwa...

Wakatoliki sasa wafikia bilioni 1.4

Picha
  -Ni katika mwaka mmoja  -Papa Francis aunda majimbo saba  Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Takwimu za Kanisa Katoliki duniani, zinaonyesha kuwa ya idadi ya Waamini wa kanisa hilo imeongezeka hadi bilioni 1.406 kufikia mwaka 2025.  Baba Mtakatifu, Papa Francis akitoa baraka kwa waumini wa kanisa hilo kwenye moja ya matukio. Kwa mujibu wa habari hizo kupitia mtandao rasmi wa Vatican, ongezeko hilo linaloihusu pia Tanzania, limemwezesha Kiongozi wa Kanisa hilo duniani, Papa Francis kuunda majimbo makuu mapya matatu; akiunda majimbo mapya saba, likiwemo Jimbo Katoliki la Bagamoyo hapa nchini. Habari hizo zimeeleza kuwa Papa Francis ameunda majimbo hayo mapya lengo kuu likiwa kusogeza huduma za kichungaji kwa watu wa Mungu mahali walipo. “Takwimu hizo zilizotolewa na Idara ya Takwimu za Kanisa Katoliki Ulimwenguni “Annuarium Statisticum Ecclesiae” zinaonesha kwamba, idadi ya Waamini wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni imeongezeka kutoka bilioni 1. 39 mwaka 2024 hadi kufi...

Waajiri watakiwa kuithamini taaluma ya Uandishi wa Habari.

Picha
Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Wamiliki wa vyombo vya Habari nchini wametakiwa kuithamini Taaluma ya Habari kwa kuwalipa stahili zao na mishahara kwa wakati waandishi wanaofanya kazi katika vyombo hivyo. Dk. Egbert Mkoko Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Dk. Egbert Mkoko, Machi 27, 2025, alipozungumza katika kipindi cha Wakeup Call,  kilichorushwa na Kituo cha Televisheni cha Upendo cha jijini Dar es Salaam. Dk. Mkoko alisema kuwa ni vyema waajiri wakatimiza wajibu wao wa kuwalipa mishahara na stahiki muhimu Waandishi wa Habari kama vile serikali itakavyowapa Ithibati ya kuwatambua kuwa hawa ni Waandishi wa Habari. "Tunatambua baadhi ya vyombo vya habari vipo hoi katika suala la uchumi kutokana na tathmini iliyofanywa mwaka uliopita ila naamini kupitia bodi ya JAB kuna kitu kitafanyika", amesema Dk. Mkoko. Amesema ni vyema waandishi wa habari na wamiliki wa vyombo hivyo wakaipa ushirikiano bodi hiyo ili iweze kufanya kazi yak...

Miaka minne ya Rais Dk. Samia, maagizo manne ya Msajili Hazina NHC 2025

Picha
  Miaka minne ya Rais Dk. Samia, maagizo  manne ya Msajili Hazina NHC 2025 -Ataja ukuaji asilimia 300 akitaka gawio zaidi kwa Serikali -Mkurugenzi NHC apambanua walipo na mwelekeo -Baraza la Wafanyakazi wajipangia makubwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wakati Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ametimiza miaka minne madarakani Machi 19,2025 akiliwezesha Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupata mfanikio ya kupigiwa mfano, shirika hilo limekamilisha Mkutano wake wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, huku Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu, akilielezea NHC kuimarika kiutendaji, uchangiaji wake serikalini kuongezeka, akiliongezea kiwango cha uchangiaji na kuifurahisha ofisi yake. Rais Dk.Samia ametimiza miaka minne madarakani akiiongoza Serikali ya Awamu ya Sita baada ya kushika hatamu ya uongozi Machi mwaka 2021, kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Rais John Pombe Magufuli, Dk. Samia  akiweka mkazo katika kuikwamua miradi ya NHC iliyokwama, ili kuwezesha watanzania wengi zaidi kupata ...

Mgodi wa Wanawake wachangia Sh. milioni 800

Picha
- Ni katika maduhuli ya Serikali - Kahama yafikia asilimia 85 ya ukusanyaji maduhuli Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com MGODI  wa Dhahabu wa Manda, unaomilikiwa na Wakinamama chini ya uenyekiti wa Asha Msangi, umechangia Shilingi Milioni 800 katika maduhuli ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025. Baadhi ya wafanyakazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Manda, Kahama wakimsikiliza Ofisa Madini  Mkazi wa Kahama, Leons Welengeile alipotembelea  mgodi huo hivi karibuni.  Mgodi huo unaendeshwa na wakinamama kwaasilimia kubwa uliopo Kahama Kijiji cha Mwime Kata ya Zongamela una leseni ya uchimbaji mdogo wa madini na umeajiri zaidi ya vijana 200. Akizungumza katika mahojiano, mmiliki wa mgodi huo ambae pia ni Mwenyekiti wa Wanawake Wachimbaji mgodini hapo, Asha Msangi amesema; “Kabla ya kuanza kwa shughuli za uchimbaji wa madini, nilikuwa nafanya biashara ndogo ndogo. Nilikuwa na kiduka kidogo, baadae nikahamia kwenye mazao, nikawa napeleka mchele Arusha. Hata hivyo, biasha...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Tumejihatiti kuboresha huduma

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imejipanga katika kuendelea kuimarisha na kuboresha uwezo wa Mawakili wa Serikali nchini. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari wakati  akizungumza kwenye mkutano maalaumu na vyombo vya habari, Machi19, 2025 ofisini kwake Kivukoni Dar es Salaam.  Hayo yamebainishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari wakati akizungumza kwenye mkutano maalaumu na vyombo vya habari, uliofanyika Machi19, 2025 ofisini kwake Kivukoni Dar es Salaam.  Akizungumza katika mkutano huo, Johari amesema ofisi yake imeandaa mafunzo maalumu kwa Mawakili wa Serikali nchini yatakayofanyika jijini Arusha Machi  24 hadi 28, 2025 yakiwa na lengo la kuongeza umahiri na utendaji kazi wa mawakili hao.  Mafunzo hayo kwa Mawakili wa Serikali ni sehemu ya kuimarisha utaratibu wa Mafunzo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa mawakili hao, pamoja na utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanz...

Serikali yavuna Shilingi Bilioni 3 ndani ya miezi 8

Picha
-Ni kupitia Sekta ya Madini Kagera  -Waita wawekezaji ndani na nje Mwandishi Wetu, daimatznews MAKUSANYO ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Kagera yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha  ulioanza Julai 2024/ 2025 ni Shilingi Bilioni 3.2. Wachimbaji madini wadogo wakiwa katika shughuli zao Kagera ilipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 5.8 na mpaka mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu wa 2025 wamefanikiwa kukusanya kiasi hicho cha fedha kikiwa ni sawa na asilimia 82 ya lengo katika kipindi cha miezi minane. Akizungumza Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kagera, Nobert Mkopi amesema fedha hizo zimekusanywa kutokana na  jitihada mbalimbali walizofanya katika usimamizi wa Sekta ya Madini katika halmashauri  zote saba za Mkoa wa Kagera. “Mkoa wa Kagera kwa maana Sekta ya  Madini tunasimamia  halmashauri zote saba kwa maana ya wilaya za Kyerwa, Karagwe, Misenyi, Muleba, Bukoba, Biharamulo na Ngara, kuna shughu...

NHC na miaka minne ya Rais Samia

Picha
 

Almasi, dhahabu vyaipaisha Shinyanga

Picha
-Yafikia 82% ya lengo ukusanyaji maduhuli* -Wawekezaji zaii waitiwa fursa  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAKUSANYO  ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Shinyanga  yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha  ulioanza Julai 2024/ 2025 ni Shilingi Bilioni 21.5. Sehemu ya mji wa Shinyanga unavyoonekana kwa picha ya juu.  Mkoa wa Shinyanga ulipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 26.2 ambapo mpaka mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu  umefanikiwa kukusanya kiasi hicho cha fedha ambacho ni sawa na asilimia 123 katika kipindi cha miezi nane na asilimia 82 ya lengo la mwaka. Akizungumza katika mahojiano maalum, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Shinyanga, Mjiolojia Daniel Mapunda amesema fedha hizo zimekusanywa kutokana na  jitihada mbalimbali walizofanya katika usimamizi wa sekta.  “Mwenendo ni mzuri, hadi kufikia mwisho wa mwaka wa fedha tuna imani tutafikia lengo,” amesema Mapunda. Aidha, Mapunda ameto...

Fuso lilipakia viroba 83 vya bangi-Korti yaelezwa

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com SHAHIDI wa Jamhuri ASP Njama amedai Fuso lililobeba mikungu ya ndizi 80 (pichani) chini lilipakia viroba 83 vya bangi. Alidai Fuso hilo walilokuwa wanalisaka lilitokea Mkoa wa Mara  lilipata  ajali maeneo ya Chamakweza wilayani Chalinze wakalikamata. ASP Njama amedai hayo Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya wakati anatoa ushahidi wa upande wa mashtaka. Mshtakiwa katika kesi hiyo, Raisan Mussa anashtakiwa kwa kukutwa na viroba 83 vyenye majani yanayosadikiwa dawa za kulevya aina ya bangi. Amedai walikuta Fuso lenye namba T223 ATC limepata ajali maeneo ya Chamakweza Chalinze wakatilia shaka kwa kuwa walikuwa na taarifa kutoka kwa msiri kuhusu gari hilo. Shahidi amedai walianza kupekua na baada ya dakika chache, Koplo George alisema juu kuna ndizi lakini chini kuna viroba vya mifuko ya salfeti akaamuru ndizi za juu zitolewe, zilishushwa zote,  ilikuwa mikungu 80. Mikungu ya ndizi...

Kesi dawa za kulevya: Shahidi adai washtakiwa hawapo kizimbani

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  SHAHIDI wa Jamhuri, E7483 Sajenti Pashua (53) ameiambia mahakama kuwa watuhumiwa wawili waliokamatwa bandarini, walikutwa na kiroba cha mchele, chenye kifurushi kilicho na chenga zilizosadikiwa kuwa dawa za kulevya aina ya heroine ndani yake. Amesema watuhumiwa hao kutoka Ofisi za Azam wanafanya kazi kupakia mizigo kwenye boti ya kwenda Zanzibar . Shahidi huyo wa Jamhuri ameeleza hayo katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Sedikia Kisanya. Shahidi huyo. aliyesema kwa sasa anafanya kazi Kituo cha Polisi Liwale tangu Desemba 2024, ambapo kabla ya kwenda huko alikuwa Kituo cha Polisi Bandari. Amesema Desemba 24 mwaka 2019 akiwa kazini katika eneo la abiria wanaokwenda Zanzibar, saa kumi jioni aliitwa na Koplo Anna aliyekuwa katika mashine ya ukaguzi wa abiria wanaotoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar. Alidai alipofika alielezwa na Koplo Anna kuwa wakati wa ukaguzi wa mizigo walikuta kiroba cha mchele, ndan...

Waziri Mkuu Mgeni rasmi miaka 30 ya VETA

Picha
Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Waziri wa Elimu,Waziri Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajia kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yatakayoanza Machi 8 hadi 21 Mwaka huu kwa kuhitimishwa katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Waziri wa Elimu,Waziri Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda akizungumzia maadhimisho ya Miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yatakayoanza Machi 8 hadi 21 Mwaka huu Mkenda amebainisha hayo jijini humo wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuitaka VETA kutengeneza mpango kazi katika kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuwezesha vijana wenye mafunzo ya ufundi stadi kuwa uwanja mpana kujiajiri na kuleta maendeleo nchini Amesema kuwa kuna mafundi ambao hawana hawajapita katika vyuo vya VETA lakini ni wabunifu ambao nao washirikishwe kupata mafunzo na kutoa ujuzi huo...