Serikali inavyoendelea kuimarisha miundombinu ya bandari

- Utendaji wa Bandari nchini waimarika kwa kipindi cha miezi saba (Mei-Novemba 2024) ikilinganishwa na (Mei-Novemba 2023) Na Mwandishi Weti, daimatznews@gmail.com. S erikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya Bandari za Dar es Salaam, Mtwara,Tanga na zile zilizopo kwenye maziwa hali iliyochangia kuongeza ufanisi katika kuhudumia shehena. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akizungumzia kuimarika kwa utendaji wa bandari nchini . Katika kipindi cha mwezi Mei 2024 hadi Novemba 2024, kiwango cha shehena kilichohudumiwa na bandari zote zilizo chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ni tani milioni 16.5 ambayo ni zaidi kwa asilimia 5.92 ya shehena milioni 15.6 iliyohudumiwa katika kipindi kama hiki mwaka uliopita (Mei 2023 hadi Novemba 2023). Kwa upande wa idadi ya Makasha yaliyohudumiwa na bandari zote zilizo chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania katika kipindi cha Mei 202...