Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Mafia Boxing Promotions yaja na Knouck Out ya Mama

Ni Boxing Day

Na Hussein Ndubikile,daimatnews@gmail.com


Kampuni ya Mafia Boxing Promotions inatarajia kufanya Mapambano 13 ya Kimatatifa ya Mchezo wa Masumbwi yaliyopewa jina la Knouck Out ya Mama yatakayofanyika Disemba 26 mwaka huu katika Ukumbi wa Superdom Masaki jijini Dar es Salaam.
Msemaji wa Kampuni ya Mafia Boxing Promotions, Jimmy Mafuvu akizungumza nawanahabari kuhusu  Mapambano 13 ya Kimatatifa ya Mchezo wa Masumbwi yaliyopewa jina la Knouck Out ya Mama yanayotarajiwa kufanyika Desemba 26,2024 katika Ukumbi wa Superdom Masaki jijini Dar es Salaam.Wengine pichani ni baadhi ya mabondia naviongoi wa kampuni hiyo

Akizungumza na wanahabari leo jijini humo Msemaji wa kampuni hiyo, Jimmy Mafuvu amesema lengo la kuyapa mapambano hayo jina la Knouck Out ya Mama ni kusapoti na kuunga mkono juhudi za kukuza sekta ya michezo zinzofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na kwamba amechangia vijana kujiajiri kupitia michezo.

" Tanzania inakwenda kupambana na mabondia mikanda mitano itapiganiwa kwa wakati mmoja hii ni mara ya kwanza mikanda hii kupiganiwa hapa nchini," amesema Mafuvu.

Amebainisha kuwa mabondia watakaopigana na mabondia wa Tanzania  wnatoka nchi za Ghana, Afrika ya Kusini na Malawi na kwamba mabondia wote wamefanya maandalizi mazuri.

Amesisitiza kuwa mabondia wa Tanzania watakaopanda ulingoni waliweka kambi ya wiki mbili nchini Afrika Kusini hivyo anaamini watashinda mapambano yao.

Ameitaja mikanda itakayopiganiwa ni WBO, WBC Africa, WBF na IBA huku akiwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi siku hiyo kushuhudia historia ikiandikwa.

Ameongeza kuwa viingilio vya mapambano hayo ni Sh 100, 000 kwa VIP,   VIP B Sh 50,000 na kawaida Sh 20,000 huku watakaohitaji kuchukua meza ya watu 10 watalipa Sh Milioni 1.5.

Kwa upande wake, Muigizaji wa Filamu, Wema Sapetu amewaomba wananchi kjitokeza kwa wingi kuunga juhudi za Rais Dkt. Samia na kwamba anategemea mabondia wa Tanzania watafanya vizuri.

Nae, Msanii wa Filamu Chuchu Hans amewahimiza Watanzania kujitokeza ili kushiriki kuandika historia katika mchezo wa masumbwi.

Muigizaji FIlamu Shamsa Ford amempogeza Rais Dkt. Samia kwa kutoa sapoti katika sekta ya michezo hasa mchezo wa ngumi na kwamba kupitia mchezo mabondia wanawake wanashiriki.

Mtangazaji wa Kituo cha Runinga cha Clouds, Sakina Lyoka amesema kuwa Rais Dkt. Samia anatambua thamani ya michezo kwani amesaidia vijana wanawake kwa wanaume kujiajiri kupitia mchezo wa ngumi.

Chapisha Maoni

0 Maoni