Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2024

Mbunge Ulanga 'alia' na Tanroads

-Sasa chumvi wauziwa Sh1,500 Mbunge wa Ulanga, ameishambulia Tanroads kwa kushindwa kutimiza wajibu wake kukarabati barabara, hivyo kuwaletea adha wananchi wa jimbo hilo iliyosababisha kupanda kwa gharama za maisha hata kununua kilo ya chumvi kwa shilingi 1,500 sasa.  Zaidi fuatilia linki hapo chini https://youtube.com/watch?v=kXBB06uSHI4&si=8xFfe0bpguIdXdpF

IPTL kuishtaki MwanaHALISI ikiwa...

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com KAMPUNI  ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) imeeleza kusudio lake kuwashtaki wamiliki, wahariri pamoja na wachapishaji wa Gazeti la MwanaHALISI  iwapo hawataomba radhi kwa kile ilichodai upotoshaji uliofanywa gazeti hilo dhidi ya IPTL. Mwanasheria wa IPTL, Leonard Manyama akisisitiza jambo, wakati akieleza kusudio la kulishtaki Gazeti MwanaHALISI, jijini Dar es Salaam . Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 28  na Wakili wa IPTL, Leonard Manyama  inaeleza kuwa hatua hiyo ya kuishtaki MwanaHALISI itafanyika kama uongozi wa  gazeti hilo utashindwa kuomba radhi, kukanusha habari hizo na kulipa fidia kama barua ya IPTL iliyowasilishwa kwa wadaiwa kupitia mawakili wake inavyowataka. Taarifa hiyo iliyotolewa na uongozi wa IPTL kupitia Wakili Manyama  inadai  kuwa gazeti MwanaHALISI kwa  nyakati tofauti limekuwa likiandika habari za kuupotosha umma dhidi ya IPTL, huku ikitaja moja ya h...

Rais Samia atunukiwa udaktari wa uchumi Uturuki

Picha
  Rais Samia Suluhu Hassan, akitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) ya Uchumi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki, Profesa Necdet Unuvar kwenye hafla iliyofanyika chuoni hapo Aprili 18, 2024.

Vyuo vikuu vyatakiwa kulinda bunifu

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Vyuo vikuu nchini vimetakiwa kulinda bunifu zinazotokana na tafiti zinazofanywa na wahadhiri na wanafunzi  nchini kwa kuzisajili, ili ziweze kuleta manufaa kwa jamii na wabunifu kwa ujumla.  Mkurugenzi wa Miliki Bunifu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Loy Mhando Mkurugenzi wa Miliki Bunifu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Loy Mhando amesema hayo wakati wa kutoa elimu na mafunzo juu ya umuhimu wa kulinda na kuzisajili bunifu wanazofanya kupitia tafiti, ili ziweze kuwaletea faida katika katika Chuo cha Waislamu Morogoro (MUM) Aprili 16, 2024. “Bunifu nyingi katika vyuo zinatokana na kazi za utafiti, zinafanyika kwa lengo la kutatua changamoto katika jamii, kazi ambazo hufanywa na wahadhiri na wanafunzi wanaojihusisha na shughuli za ubunifu zikiwemo uandishi, ambapo tafiti  zao huleta matokeo katika kutatua matatizo kwenye jamii,” amesema Loy. Amebainisha kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwaelez...

Iran yatoa msimamo dhidi ya Israel

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa msimamo wa kutumia haki ya kujilinda kiasili chini ya Sheria ya Kimataifa na kusisitiza kwamba haifanyi kazi ya kuongeza au kusambaza mgogoro, huku ikionya kuhusu machafuko zaidi ya kijeshi, yanayoweza kusababishwa na utawala wa Israeli. Kiongozi Mkuu wa kidini wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei Hayo yamebainishwa katika taarifa ilitolewa jana kwa vyombo vya habari na Serikali ya Iran kupitia Mtaalamu wa Ushauri wa Kitamaduni wa Ubalozi wa Iran nchini,Maulid Sengi. "Tunatoa msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kuhusu kutumia haki yake ya kujilinda kiasili chini ya Sheria ya Kimataifa, kujibu mashambulizi ya kijeshi ya utawala wa Israeli, dhidi ya majengo ya kidiplomasia ya Iran huko Syria," amesema Sengi na kuongeza; "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inarudia msimamo wake thabiti kwamba, haifanyi kazi ya kuongeza au kusambaza mgogoro katika eneo, inaonya kuhusu machafuko zaidi ya kijeshi yanayoweza kus...

'Maendeleo yanavyotafuna vijana kimaadili'

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ukuaji wa utandawazi umetajwa kuchangia kundi kubwa la vijana nchini kutokana na kukua na kuenea kwa sayansi na teknolojia inayogusa kwa karibu vijana, ikielezwa sehemu kubwa ya kundi hilo limetafunwa na maendeleo hayo kwa kupotoka kimadili. Mkufunzi wa Shirika la Kutetea Uhai Tanzania (ProLifeTz), Godfrey Mkaikuta pichani juu, amesema hayo Aprili 16, 2024 wakati akijadili Mada ya Maisha ya Vijana katika Dunia ya Leo, iliyoandaliwa na ProLifeTz kwa vijana wa Jimbo Katoliki Ifakara. "Wazazi na walezi wa Tanzania, ulimwengu unatudai kubaki katika msingi wa malezi ya tamaduni na asili za kiafrika kwa kuwafanya vijana na watoto kupenda na kuheshimu maadili yao, pia kujiepusha na tamaduni za mataifa ya nje," amesema Mkaikuta. Katika tafakari yake, Mkaikuta amesema vijana wengi wameutoa utu wao wa ndani waliopewa na Mungu kwa kukimbilia mambo ya kigeni, wakijidanganya kwamba ni mabadiliko na ukuaji wa sayansi na teknolojia. "Ifike pahali...

Mfanyakazi benki adaiwa kupiga mtu nyundo

Picha
-Akutwa na kesi ya kujibu   Mwandishi Wetu,daimatzanews@gmail.com   MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam imemkuta na kesi ya kujibu mfanyakazi wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi, anayetuhumiwa kumjeruhi kwa nyundo jirani yake, Deogratus Minja kwa madai kuwa alikwenda kumshitaki Serikali za Mitaa kwa kutiririsha maji machafu mbele ya nyumba yake. Akitoa uamuzi huo leo, Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Amos Rweikiza amesema mahakama baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wote imeridhika kwamba mshitakiwa ana kesi ya kujibu kwa hiyo atatakiwa kujitetea.    Hakimu Rweikiza alimueleza mshitakiwa: "Pamoja na kukutwa na kesi ya kujibu, una haki ya kuleta mashahidi na vielelezo wakati wa kujitetea, pia unaweza kutoa ushahidi wako chini ya kiapo au ukitaka, anaweza kukaa kimya," amesema Hakimu.   Baada ya hakimu kusema hayo, wakili wa mshitakiwa alidai kuwa mteja wake atajitetea chini ya kiapo, pia hatokuwa na shahidi wala vielelezo vyovyote na ...

TRAMPA mguu sawa yapiga msasa watumishi wa umma

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mwenyekiti wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA), Devotha Mrope amezindua mafunzo maalumu yanayolenga kujenga uwezo wa kitaaluma kwa wataalamu utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka nchini. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Devotha amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha watumishi wa umma na taasisi binafsi kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na uadilifu katika utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka.   Mwenyekiti wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania  (TRAMPA), Devotha Mrope "Mafunzo haya yatawakilisha juhudi za TRAMPA katika kujenga uwezo na kuimarisha mifumo ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka nchini Tanzania. Tunajitahidi kuhakikisha wataalamu wetu wanapata mafunzo na maarifa yanayohitajika ili kuhakikisha taarifa na nyaraka zinatunzwa kwa weledi na uadilifu,"  amesema Devota. Mwenyekiti huyo wa TRAMPA amebainisha kuwa mafunzo hayo yamepangwa kufanyika tena Mei 6 hadi 9...

'Serikali kuboresha mazingira ya biashara'

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji amesema Serikali ya awamu ya Sita imedhamiria kuboresha na kuimarisha mazingira ya biashara nchini ili kuendana na azma ya kufanya mageuzi ya kiuchumi na viwanda lengo likiwa kuleta maendeleo endelevu ya jamii. Waziri wa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji   Dk. Kijaji amesema hayo  Aprili 6, 2024 alipokuwa akifungua kikao cha Wizara hiyo na Wakuu wa Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kilichofanyika mkoani Morogoro. "Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan itaendeleza jitihada zake katika kujenga uhusiano mzuri na wafanyabiashara ili kukuza uchimi wa Taifa," amesema. Ameongeza: “Dunia imeshaingia katika mapinduzi ya nne ya viwanda ambayo yanajikita katika matumizi makubwa ya teknolojia na utoaji wa huduma kwa haraka, watu kukutana kidigitali na uwepo wa maarifa ya kutosha na b...

FinScope: Asilimia 36 ya Wazanzibar ni tegemezi

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Zaidi ya theluthi ya wananchi wa Zanzibar ni tegemezi, huku asilimia 23 ya wakazi hao wakiishi kwa kutegemea vibarua, matokeo ya utafiti wa FinScope Tanzania 2023 kwa Zanzibar   yamebainisha. FinScope Tanzania ni utafiti wa kina wa mahitaji ya sekta ya fedha kwa watu wazima Tanzania, walio na umri wa kuanzia miaka 16 na kuendelea. Kwa mujibu wa matokeo hayo, katika kipengere cha vyanzo vya mapato, asilimia 17 ya Wazanzibar ni wafanyabiashara,   wanaopokea mishahara ni asilimia tisa, wakulima asilimia nane na makundi mengine asilimia sita. Dk. Saada Mkuya Salum, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango  wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Hali hiyo inaweza kutafsiriwa kwamba licha ya juhudi kubwa za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuendeleza wananchi wake, juhudi zaidi zinahitajia katika kupanga, kusimamia na kutekeleza mipango ya kiuchumi na maendeleo inayowahusu moja kwa moja wananchi wa Zanzibar, ili kuondokana na hali hiy...

LHRC yachambua sheria uchaguzi

Picha
-Yataka Muswada Katiba bungeni    Mwandishi Wetu, daimatzanews@gmail.com  KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimechambua Sheria za Uchaguzi zilizosainiwa hivi karibuni na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kikieleza kuwa kimehusika kikamilifu katika jitihada za uchechemuzi na maboresho ya mfumo wa uchaguzi na vyama vya siasa nchini, huku ikitoa wito kwa Serikali kuwasilisha Bungeni Muswada wa Mabadiliko ya Katiba kwa manufaa ya watanzania.  Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Aprili 4, 2024 mbele ya wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk. Anna Henga amebainisha kwamba kituo hicho kilihusika katika mchakato wa maboresho ya Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya 2024, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya 2024, Sheria ya Vyama vya Siasa na Gharama za Uchaguzi, zilizopitishwa na Bunge kisha kusainiwa na Rais. Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk. Anna Henga akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 4, 2024 jijini Dar es Salaam.  "Tamko h...

Rais Dk Samia: Taasisi zote zisajiliwe kabla Desemba

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Rais Samia Suluhu Hassan ameiagiza Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) kuhakikisha inasajili taasisi zote za umma na binafsi kabla ya Desemba mwaka huu. Rais pia ameitaka Ofisi ya Waziri Mkuu, kuhakikisha mifumo yote ya Tehama iwe inasomana ndani ya kipindi hicho mwaka huu. Ametoa maagizo hayo leo Aprili 3, 2024 wakati akizindua tume hiyo pamoja na mifumo ya usajili na malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya ulinzi wa taarifa binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan akigusa screen ya iPad kuashiria uzinduzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na Mifumo ya Usajili na Malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam Aprili 3, 2024. “Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ihakikishe taasisi zote za umma na binafsi zinapaswa kusajiliwa. Zinasajiliwa na kutekeleza Sheri...