Wagombea udiwani 16 Kigoma wakosa wapinzani
- Samia kunguruma Septemba 13 -Ndalichako kuwasha moto Sept 4 -Prof Yanga hapoi Mwandishi Wetu, Kigoma Wagombea udiwani 16 kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kigoma wamebahatika kuwania nafasi hizo bila kupingwa, baada ya vyama vingine vya siasa mkoani humo kushindwa kusimamisha wagombea, huku kwenye baadhi ya kata wagombea wa upinzani wakielezwa kukosa sifa. Rais Dk.Samia Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, akizungumza katika moja ya mikutano yake. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo CCM Mkoa wa Kigoma, Deogratius Nsokolo amebainisha hali hiyo akieleza kuwa kwa CCM hiyo ni dalili njema ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao Oktoba 29, 2025, ambapo sasa wagombea hao wanasubiri kupigiwa kura za ndiyo na hapana. Nsokolo amezitaja kata hizo ambazo wagombea wa CCM wamekosa upinzani ni pamoja na zilizopo Wilaya ya Kasulu ambapo wagombea sita waliokosa wapinzani, Wilaya ya Buhigwe kata tano, Wilaya ya Kibondo kata nne na Uvinza ikiwa kata moja ya Basanza. "M...