Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2025

Wagombea udiwani 16 Kigoma wakosa wapinzani

Picha
- Samia kunguruma Septemba 13 -Ndalichako kuwasha moto Sept 4 -Prof Yanga hapoi Mwandishi Wetu, Kigoma Wagombea udiwani 16 kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kigoma wamebahatika kuwania nafasi hizo bila kupingwa, baada ya vyama vingine vya siasa mkoani humo kushindwa kusimamisha wagombea, huku kwenye baadhi ya kata wagombea wa upinzani wakielezwa kukosa sifa. Rais Dk.Samia Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, akizungumza katika moja ya mikutano yake. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo CCM Mkoa wa Kigoma, Deogratius Nsokolo amebainisha hali hiyo akieleza kuwa kwa CCM hiyo ni dalili njema ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao Oktoba 29, 2025, ambapo sasa wagombea hao wanasubiri kupigiwa kura za ndiyo na hapana. Nsokolo amezitaja kata hizo ambazo wagombea wa CCM wamekosa upinzani ni pamoja na zilizopo Wilaya ya Kasulu ambapo wagombea sita waliokosa wapinzani, Wilaya ya Buhigwe kata tano, Wilaya ya Kibondo  kata nne na Uvinza ikiwa kata moja ya Basanza. "M...

BRELA ilivyojizatiti utoaji elimu, kusimamia Sheria ya Miliki Bunifu

Picha
- Usajili wapaa - Miliki Bunifu 7 zasajiliwa kila siku ndani ya siku 365  - Hataza 30 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ( BRELA ), umejidhatiti kutoa elimu kwa wananchi, wasanii, wabunifu, watafiti na taasisi mbalimbali nchini kuhusu umuhimu wa kulinda na kusajili bunifu, sambamba na kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Miliki Bunifu. Waziri wa Viwanda na Biashara, Selemani Jafo(aliyeketi kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa kuhusu utendaji BRELA . Hatua hiyo inalenga kuhakikisha wabunifu wananufaika na kazi zao, kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Miliki Bunifu nguzo ya maendeleo Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Miliki Bunifu Duniani yaliyofanyika Mei 21, 2025 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dk. Selemani Jafo amesisitiza umuhimu wa wabunifu, wajasiriamali na wasanii kusajili bunifu zao ili kulinda haki zao kisheria....

NHC yapata tuzo maalum vigezo vitano vikiibeba

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limetunukiwa tuzo maalum, baada ya kuibuka kuwa moja ya mashirika   ya umma yaliyofanya vizuri katika mwaka wa fedha 2023/24. Tuzo hiyo imetolewa na Ofisi ya Msajili wa Hazina katika hafla rasmi iliyofanyika kwenye Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma, kilichofunguliwa rasmi Agosti 2,2025 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Philip Mpango, jijini Arusha. Tuzo hizo zilizingatia vigezo vya kiuendeshaji ikiwamo ukuaji wa mapato ya ndani, kuboresha ukwasi, rejesho la uwekezaji, udhibiti wa matumizi na kuimarisha faida. Vigezo vingine ni kupunguza utegemezi wa ruzuku ya Serikali, ufanisi katika matumizi, utekelezaji wa hoja za kikaguzi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), uchapishaji wa taarifa za fedha, na maboresho ya utoaji huduma kwa jamii. Taasisi nyingine zilizotunukiwa tuzo maalum zilitangazwa chini ya makundi manne mahsusi kuli...

Rais Samia ahimiza kudumisha amani, haki kuelekea Uchaguzi Mkuu

Picha
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema upo umuhimu wa kuhakikisha Taifa linaendelea kudumu katika misingi imara ya haki, amani, umoja na mshikamano wa kitaifa iliyowekwa na waasisi wa Tanzania , akieleza kwamba ili kudumisha misingi hiyo ushirikiano na mshikamano wa viongozi wa dini ni nguzo muhimu. Rais Dk. Samia akizungumza katika  Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Ameeleza hayo katika hotuba yake leo Agosti 24, 2025 kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ambalo liliandalia na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) na Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania. Taarifa Ikulu iliyotolewa na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Shaaban Kissu imeeleza kuwa Rais Dk. Samia amesema uchaguzi ni fursa ya kidemokrasia inayopaswa kwenda sambamba na kulinda amani na utulivu wa taifa.   “Kudumisha amani ni utamaduni wetu tuliojijengea katika demokrasia ya uchaguzi. Tuendeleze utamaduni huu kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu,” am...

Miezi 24 ya BRELA kuipigania Sheria ya Umiliki Manufaa

Picha
   -- Yawafunda wamiliki wa kampuni, mawakili -  Yaziwezesha taasisi za uchunguzi wa uhalifu kukabiliana na tatizo hilo Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika harakati za kuimarisha uwazi na uwajibikaji kwenye sekta ya biashara na makampuni nchini, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umechukua hatua thabiti ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu wa kifedha na utambuzi, kuhusu utambuzi wa wamiliki manufaa wa kampuni na majina ya biashara. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA),  Godfrey Nyaisa akikabidhi Tuzo kwa wafanyakazi wa  taasisi hiyo iliyotunukiwa baada ya kutoa gawio kwa Serikali la Shilingi Bilioni 20.4  kwa mwaka 2024. BRELA imepata Tuzo hiyo katika kipengele cha Taasisi zilizofanya vizuri kwa utoaji gawio kwa wakati kwa mwaka 2025 . BRELA imeeleza kuwa hatua hizo ni utekelezaji wa Pendekezo Na. 24 la Kundi Kazi la Kimataifa la Kupambana na Uhalifu wa Kifedha (FATF), linalosisitiza uwazi katika ...

Miezi 24 ya BRELA kuipigania Sheria ya Umiliki Manufaa

Picha
 -- Yawafunda wamiliki wa kampuni, mawakili -  Yaziwezesha taasisi za uchunguzi wa uhalifu kukabiliana na tatizo hilo Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika harakati za kuimarisha uwazi na uwajibikaji kwenye sekta ya biashara na makampuni nchini, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umechukua hatua thabiti ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu wa kifedha na utambuzi, kuhusu utambuzi wa wamiliki manufaa wa kampuni na majina ya biashara. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA),  Godfrey Nyaisa akikabidhi Tuzo kwa wafanyakazi wa  taasisi hiyo iliyotunukiwa baada ya kutoa gawio kwa Serikali la Shilingi Bilioni 20.4  kwa mwaka 2024. BRELA imepata Tuzo hiyo katika kipengele cha Taasisi zilizofanya vizuri kwa utoaji gawio kwa wakati kwa mwaka 2025 . BRELA imeeleza kuwa hatua hizo ni utekelezaji wa Pendekezo Na. 24 la Kundi Kazi la Kimataifa la Kupambana na Uhalifu wa Kifedha (FATF), linalosisitiza uwazi katika umili...

Saa 144 za CCM kutaja kikosi chake bungeni

Picha
-Wagombea presha inapanda, presha inashuka Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Saa 148 zimesalia kuanzia leo Agosti 18, kabla ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutangaza majina ya wateule wake kwa nafasi za ubunge watakaochuana na wagombea vyama vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu ujao Oktoba 29, 2025 ili kuingia bungeni.   Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dk. Samia Suluhu Hassan Muda huo ambao ni sawa na siku sita, unawaacha wagombea waliopita kwenye kura za maoni ngazi ya jimbo, presha zao zikipanda na kushuka, wakisubiri kwa hamu uamuzi wa vikao vya kitaifa vya CCM vya uteuzi, ambavyo uamuzi wake ni wa mwisho. Vikao hivyo vinafanyika huku kukiwa na kumbukumbu ya baadhi ya wagombea majina yao kutorudi kwenye mchujo wa awali mwaka huu, lakini pia kuwepo waliokatwa kwenye uteuzi wa mwisho katika vikao kama hivyo, mwaka 2020 ambapo CCM ilikuwa chini ya uenyekiti wa hayati John Magufuli, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   Ago...

Samia Housing Scheme Kawe: Ndoto makazi bora ya kisasa imetimia

Picha
-Kutoka wazo, ramani hadi uhalisia -Wamiliki wapigwa msasa, waanza kukabidhiwa nyumba zao Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Barabara zimekamilika, mifereji ya maji safi na maji taka iko tayari, taa za barabarani na kamera za usalama zimeshawekwa, huku bustani na miti michache ikipamba mitaa na kuleta utulivu.  Ukiwa maeneo hayo asubuhi utashuhudia jua linapochomoza, lakini jioni jua linapozama juu ya majengo hayo mapya, likiongeza mvuto wa rangi za nyumba hizo mpya zilivyopangiliwa kwa umaridadi, zisizochosha kutazama. Eneo hilo pia lina vizuia moto, mifumo ya kisasa ya utiririshaji maji na barabara za ndani  zilizokamilika, mitandao ya umeme imetengenezwa, na maeneo ya kijamii yameundwa kwa ustadi, pamoja na bustani. Mradi huo  wenye nyumba 560 unaunganisha maisha ya kisasa, faraja, na mshikamano wa kijamii, lakini pia kutoa mwonekano unaochochea hisia za kifahari.  NHC sio tu limekamilisha mradi huo, bali pia siku limeanza kukabidhi kwa wamiliki wake nyumba hiz...

Serikali sasa kusaini muongozo mshahara KCC kwa Sekta Binafsi

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com SERIKALI imesema hivi karibuni inatarajia kusaini muongozo wa Kima Cha Chini Cha Mshahara (KCC) kwa TaasisiI Minafsi zinazofanywa kazi nchini, ili kuwa sheria. Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira  Vijana na Wenye Ulemavu, Ridhiwan Kikwete. Imesema katika miongozo huo inatarajia kuainisha viwango vipya vya mshahara ambapo wafanyakazi Wa sekta binafsi watakuwa wanalipwa. Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira  Vijana na Wenye Ulemavu, Ridhiwan Kikwete amesema hayo jijini Arusha katika uzinduzi wa Jengo la Biashara Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), lililoko mkabala na soko kuu, jijini humo. Kuhusu miongozo huo Ridhiwan amesema tayari mazungumzo yameshafanyika baina ya wadau ambao ni taasisi binafsi na wasimamizi wa sera, pamoja na uongozi wa timu Ya Wizara uliopewa jukumu la kusimamia marekebisho hayo. Amesema kikao kilichobakia ni cha mashauri ,ambapo watashauriana na wenzao juu ya viwango vilivyowekwa ...

Waomba kuondolewa vikwazo biashara ya mazao ya kilimo Ikolojia mipakani

Picha
Mussa Juma,Arusha Serikali katika nchi za Afrika ya Mashariki, zimeombwa kuondoa vikwazo vinayoathiri biashara za mazao ya kilimo Ikololojia mipakani, hasa kwa wajasiriamali wadogo, ili kuwezesha kukuza biashara hiyo. Utafiti uliofanywa kuhusu biashara za kilimo Ikolojia (Kilimo Hai) mipakani zimebaini kuwepo kwa changamoto kadhaa ikiwemo viwango vya ubora wa bidhaa,mifumo ya ulipaji kodi,vikwazo vya barabarani,udhibiti wa bidhaa zisizo na ubora na uelewa mdogo wa wajasiriamali katika masuala ya biashara ya mipakani. Akisoma mapendekezo ya kisera yaliyotokana na  warsha ya wadau kuhusu biashara  ya mipakani kwa mazao ya bidhaa za kilimo Ikolojia, Ofisa wa Utetezi na Ushawishi wa Shirikisho la  Wakulima Tanzania (SHIWAKUTA), Thomas Laizer amesema   wamekubaliana kuwa ni  muhimu, kuchukuliwa hatua madhubuti ili kuondoa au kupunguza vikwazo visivyo vya kikodi (NTBs), ikiwemo mazuio yasiyo rasmi ya barabarani, ambayo kwa kiasi kikubwa inaathiri biashara za mipa...

Job Ndugai afariki dunia

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Spika wa Bunge la 12, Job Ndugai amefariki dunia, jijini Dodoma. Marehemu Job Ndugai Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imemnukuu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ikieleza kuwa Spika mstaafu, Ndugai ambaye alikuwa Mbunge wa Kongwa, amefariki dunia leo Agost 6 mwaka 2025. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Ndugai amefariki wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika moja ya hospitali jijini Dodoma. "Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea leo jijini Dodoma. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Kongwa. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira kipindi hiki kigumu," amesema Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson. Spika mstaafu Ndugai amefariki dunia siku moja baada ya kutangazwa kushinda kura za maoni kuwania tena kiti cha Ubunge Jimbo la Kongwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), n...