Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2025

Job Ndugai afariki dunia

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Spika wa Bunge la 12, Job Ndugai amefariki dunia, jijini Dodoma. Marehemu Job Ndugai Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imemnukuu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ikieleza kuwa Spika mstaafu, Ndugai ambaye alikuwa Mbunge wa Kongwa, amefariki dunia leo Agost 6 mwaka 2025. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Ndugai amefariki wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika moja ya hospitali jijini Dodoma. "Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea leo jijini Dodoma. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Kongwa. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira kipindi hiki kigumu," amesema Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson. Spika mstaafu Ndugai amefariki dunia siku moja baada ya kutangazwa kushinda kura za maoni kuwania tena kiti cha Ubunge Jimbo la Kongwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), n...

Majangili wabanwa Ranchi ya Mwiba, Pori la Akiba la Maswa

Picha
Mwandishi Wetu,Meatu  Ushirikiano baina ya Askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori nchini (TAWA) Taasisi ya Uhifadhi ya Mwiba Holdings na Askari wa Wanyamapori wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Mara, umefanikisha kudhibiti watukio ya ujangili katika eneo la pori la Akiba la Maswa na Ranchi ya Mwiba. Wakizungumza katika Maadhimisho ya Kimataifa la Walinzi wa Wanyamapori Duniani Agosti 5-2025 kwa lengo la kuenzi kazi nzuri inayofanyika na walinzi wa wanyamapori, Askari wa Wanyamapori, wamesema wanaadhimisha siku hiuo kwa mara ya kwanza wilayani Meatu, wakiwa na faraja kubwa kudhibiti ujangili. Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi cha Kampuni ya Mwiba Holdings, iliyo chini ya Taasisi ya Friedkin Conservation Fund, waliowekeza katika Pori la Akiba la Maswa na Ranchi ya Mwiba,Steve Alexander amesema ushirikiano baina yao na TAWA umekuwa na manufaa. Alexander ambaye ni mbombezi katika masuala ulinzi wa wanyamapori, amesema kutokana na ushirikiano huo sasa matukio ya majangili wakubwa wa ...

Mikakati, miradi ya NHC 2025-2026 iliyowasilisha kwa Waziri wa Ardhi hii hapa

Picha
  -  Ni ujenzi wa makazi, mifumo ya kibiashara wapaa -Yaja na majawabu changamoto upungufu nyumba bora -Yaendelea kuwa kinara miradi ya kimkakati  Mwandishi Wetu,   daimatznews@gmail.com Katika kipindi hiki ambapo Tanzania inawekeza kwa kasi katika maendeleo ya miundombinu, ustawi wa jamii na ukuaji wa uchumi jumuishi, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limewasilisha taarifa ya miradi na mwelekeo wa mikakati yake mbele ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Deogratius Ndejembi, huku  likiendelea kuwa chombo muhimu katika kusukuma mbele ajenda ya Taifa ya makazi bora kwa Watanzania wote.  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Deogratius Ndejembi NHC imetekeleza hilo h ivi karibuni, wakati Waziri  Ndejembi, alipotembelea Makao Makuu ya NHC, aki ongozana na uongozi wa juu wa wizara,ambapo alikutana na menejimenti ya NHC kwa lengo la kujionea hatua za utekelezaji wa miradi mbalimbali na kutoa mwongozo wa kisera. Katika ziara...

KUTOPIGA MSWAKI IPASAVYO CHANZO CHA MAGONJWA YA FIZI – DK. KAHAMBA

Picha
Kutopiga mswaki ipasavyo kumetajwa kuwa ni chanzo cha magonjwa ya fizi, yanayowakabili watu wengi bila wenyewe kufahamu, huku wakiaswa kupiga mswaki ipasavyo ili kuepuka tatizo hilo. Dk. Jawadu Kahamba Rai hiyo imetolewa na Mtaalam wa Kinywa na Meno, Dk.  Jawadu Kahamba  kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera, wakati akitoa elimu ya kinywa na meno kupitia Kitengo cha Habari na Uhusiano cha hospitali hiyo. Dk. Kahamba amesema kuwa watu wamekuwa wakikumbwa na magonjwa ya fizi kutokana na kutopiga mswaki ipasavyo na kutotumia dawa ya meno yenye madini ya kulinda fizi, yakiwemo fluoride. “Kutopiga mswakiipasavyo na kutotumia dawa zinazolinda fizi ni tatizo kubwa linalosababisha magonjwa ya fizi. Mtu anatakiwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku, yaani asubuhi na usiku kabla ya kulala. Hiyo ndio hali ya kawaida,” amesema Dk. Kahamba. Ametaja sababu nyingine za watu kupatwa na magonjwa ya fizi kuwa ni uvutaji wa sigara, ulaji wa ugoro pamoja na ulaji hafifu wa vyakula vyenye madi...