Job Ndugai afariki dunia

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Spika wa Bunge la 12, Job Ndugai amefariki dunia, jijini Dodoma. Marehemu Job Ndugai Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imemnukuu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ikieleza kuwa Spika mstaafu, Ndugai ambaye alikuwa Mbunge wa Kongwa, amefariki dunia leo Agost 6 mwaka 2025. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Ndugai amefariki wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika moja ya hospitali jijini Dodoma. "Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea leo jijini Dodoma. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Kongwa. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira kipindi hiki kigumu," amesema Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson. Spika mstaafu Ndugai amefariki dunia siku moja baada ya kutangazwa kushinda kura za maoni kuwania tena kiti cha Ubunge Jimbo la Kongwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), n...