Majengo, eneo Urafiki vyauzwa kwa NHC

-NHC yalipa mabilioni - Ni kupitia mnada wa wazi, sasa mandhari kuboreshwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limenunua rasmi eneo la Urafiki na majengo yaliyokuwa chini ya Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD). Sehemu ya majengo ya kilichokuwa la kiwanda cha Urafiki, ambayo sasa ni mali ya NHC. Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya ameyasema hayo leo wakati wa ziara ya kukagua maeneo mbalimbali, ambayo sasa yatakuwa chini ya miliki ya NHC na kufafanua kuwa eneo hilo linajumuisha nyumba, maghala, viwanja vya wazi, viwanda na mali nyinginezo. Katika ziara yake, Saguya ameelezea furaha yake na matumaini makubwa kuhusu hatua hiyo, akibainisha kwamba itasaidia kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa maeneo hayo ikiwamo kuboresha mandhari ya Dar es Salaam. Amesema kuwa NHC, imelinunua eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 50 kutoka kwa mnada wa wazi kiki...