Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2024

Majengo, eneo Urafiki vyauzwa kwa NHC

Picha
 -NHC yalipa mabilioni - Ni kupitia mnada wa wazi, sasa mandhari kuboreshwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limenunua rasmi eneo la Urafiki na majengo yaliyokuwa chini ya Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD).  Sehemu ya majengo ya kilichokuwa la kiwanda cha Urafiki, ambayo sasa ni mali ya NHC. Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya ameyasema hayo leo wakati wa ziara ya kukagua maeneo mbalimbali, ambayo sasa yatakuwa chini ya miliki ya NHC na kufafanua kuwa eneo hilo linajumuisha nyumba, maghala, viwanja vya wazi, viwanda na mali nyinginezo. Katika ziara yake, Saguya ameelezea furaha yake na matumaini makubwa kuhusu hatua hiyo, akibainisha kwamba itasaidia kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa maeneo hayo ikiwamo kuboresha mandhari ya Dar es Salaam. Amesema kuwa NHC, imelinunua eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 50 kutoka kwa mnada wa wazi kiki...

Nape: 2024/2025 tutatekeleza haya

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, imebainisha malengo 28 itakayotekeleza katika mwaka wa fedha 2024/25 ikiwamo kujenga Kituo cha kuhifadhi Data Dodoma na Zanzibar, pamoja na kuanzisha kituo kimoja cha Usalama wa Mawasiliano cha Taifa. Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye akiwasilisha bungeni, makadirio ya bajeti, mapato na matumizi ya wizara yake lo Mei16, 2024. Waziri wa wizara hiyo, Nape Nnauye, amebainisha hayo wakati akiwasilisha Bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2024/25, bungeni mjini Dodoma leo Mei 16, 2024. "Serikali pia imepanga kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano na vyombo vya ulinzi na usalama kama Mahakama, TAKUKURU, Polisi, Magereza, JWTZ, Usalama wa Taifa), pamoja na taasisi 100 za Haki Jinai na Taasisi nyingine za Serikali," amesema Waziri Nape.             Ametaja mambo mengine yatakayotekelezwa kuwa ni ukamilishaji wa ujenzi wa minara ya mawasilia...

Waziri Nape, Mhandisi Maryprisca walivyopongezwa bungeni

Picha
 Picha mbalimbali zikionyesha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (Mb) na Naibu Waziri wake, Mhandisi Maryprisca Mahundi wakipongezwa baada ya kupitishwa kwa Bajeti, Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka 2024/2025 bungeni jijini Dodoma leo, Mei 16, 2024. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa(kulia), akimpongeza  Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (Mb), baada ya wabunge kupitisha Bajeti na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo, Mei 16, 2024 bungeni Dodoma.   Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko akimpongeza  Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (kushoto), baada ya wabunge kupitisha Bajeti na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo, Mei 16, 2024 bungeni Dodoma Pichani juu na chini; Mawaziri na wabunge mbalimbali wakimpongeza Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (Mb) na Naibu Waziri wa Wi...

Wizara ya Habari kukusanya Sh. bilioni 100

Picha
Waziri Nape aomba Sh. bilioni 180 za matumizi Mwandishi Wetu,  Wazara ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, inatarajia kukusanya zaidi Sh. Bilioni 100.7 (100,700,000,000) kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato vya wizara hiyo ikiwemo mauzo ya huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, huku ikiliomba Bunge, kuidhinisha kiasi cha Sh. bilioni 180.9 kwa ajili ya matumizi ya wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/25. Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye akiwasilisha bajeti ya wizara yake bungeni mjini Dodoma leo, Mei 16,2024 Wazara ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye ameeleza hayo leo Mei 16, 2024 bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025.   Kwa mujibu wa Waziri Nape, makusanyo mengine ya wizara hiyo kwa ujao wa fedha yatatokana na ada ya usajili wa Magazeti, ada ya mwaka ya magazeti, vitambulisho vya waandishi wa habari na machapisho ya picha...

Iran yakumbuka mateso ya uzayuni, yalaani

Picha
-Ni Siku ya Nakbat, yalaani ubeberu Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com KITUO cha Utamaduni cha Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo Mei 16,2024 kinaadhimisha miaka 76 kukumbuka siku ya Nakbat, tangu kuanzishwa kwa utawala wa ubaguzi wa rangi na uvamizi kwenye ulimwengu wa Kiislamu. Picha ikionyesha Wapalestina wakihangaika kutafuta makazi, baada ya  kuanzishwa kwa utawala wa ubaguzi wa rangi na uvamizi wa Kizayuni enzi hizo. Picha kwa hisani ya Ubalozi wa Iran   Akizungumza na waandishi wa Habari Dar es Salaam leo, Mtaalamu wa Utamaduni wa Kituo hicho, Maulid Sengi amesema awali wakati wa mzozo, Wazayuni walishambulia kwa ukatili miji na vijiji vya Wapalestina na kuua maelfu ya raia wa Kiislamu na Kikristo. “Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilitoa tamko kwa ajili ya kuadhimisha tukio hilo *Siku ya Nakba 1403* lililosema; "Siku ya Nakba inaadhimisha kumbukumbu ya kuanzishwa kwa utawala wa ubaguzi wa rangi na uvamizi wa Kizayuni katikati ya ulimweng...

Hatifungani Kijani Tanga UWASA zasajiliwa DSE

Picha
- Waziri azielekeza taasisi nyingine kutumia utaratibu huo Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Hatifungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga inayosimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA), imesajiliwa rasmi katika Soko la Hisa la Dar es Salaam(DSE). Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Kushoto),akiteta jambo na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso wakati wa hafla ya kusajiliwa Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE),kwa  Hatifungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga inayosimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA), leo Mei 15,2024. Zoezi hilo limefanyika katika hafla maalumu iliyofanyika jijini Dodoma katika Ofisi za Hazina, baada ya mauzo ya Hatifungani hiyo kufanya vizuri kwa asilimia 103 ikiwa ni zaidi ya lengo kusudiwa. Akizungumza katika hafla hiyo, mgeni rasmi , Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa aliyezungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba  amezielekeza taasisi nyingine za Serikali kutumia utara...

CRDB yatajwa orodha benki bora duniani 2024

Picha
 -Yatajwa pekee kwa Tanzania Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com CRDB imetajwa kuwa benki bora zaidi nchini, iking'ara Afrika Mashariki na kutajwa miongoni mwa benki bora barani Afrika mwaka 2024. Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela Kwa mujibu wa Mtandao wa Kimataifa Global News, Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha Duniani (IMF), zimeitaja CRDB pia kuwa miongoni mwa benki bora duniani kwa mwaka huu 2024 ukanda wa Afrika. Kwa mujibu wa mtandao huo uliochapisha habari hizo mapema mwezi huu Mei,2024, kulichoipaisha CRDB kuingia kwenye benki ubora ni uwekezaji wake endelevu wa dola milioni 300 (Tsh 780, bilioni) katika eneo uhifadhi mazingira, kupitia mpango wake wa Kijani Bond. Kwa ukanda wa Afrika Mashariki, nchini Uganda Centenary Bank imetajwa kuwa mshindi wa ubora, wakati ambapo imeadhimisha mika 40 mwaka uliopita 2023 ikiwa na wateja milioni 2.4 huku ikikua kwa kasi. Kwa mwaka huu, mshindi kutoka nchini Kenya ni Co-operative Bank, inayotajwa kuwa ...

Brela, Z’bar zafaidi

Picha
  - F aida nne sheria kuzikutanisha, m afanikio lukuki Miliki Bunifu,  -Ni matunda ya miaka 60 ya Muungano Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wakati taifa likiadhimisha miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, mwaka huu 2024, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), umeitaja Sheria ya Taifa ya Usajili na Utoaji wa Leseni za Viwanda Sura ya 46, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 kuwa ndiyo iliyoleta muungano wa kiutendaji baina yake na Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda ya Zanzibar na sasa wote wanafaidi. Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa . Nchi hizo huru, ziliungana Aprili 26.1964 ambapo Mwalimu Julius Nyerere akawa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume, akawa Makamu wa Rais.  Akizungumzia miaka 60 ya muungano, Afisa Mtendaji Mkuu wa Brela, Godfrey Nyaisa amesema kuundwa kwa sheria hiyo kumewezesha pande mbili za muungano kufanya kazi pamoja ambapo sasa inasimamiwa ...

Waziri mstaafu afariki dunia

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Fedha wa zamani Mustafa Mkulo(77), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa. Marehemu Mustafa Mkulo, enzi za uhai wake, akijibu maswali bungeni. Picha kwa hisani ya Mtandao . Taarifa za kifo cha Mkulo aliyeshika wadhifa huo kati ya mwaka 2007 hadi 2012, zinamnukuu mke wa marehemu, Julie akitangaza kuwa kimetokea Mei 3. Kwa mujibu wa tangazo la familia ya Mkulo shughuli za mazishi zitafanyika nyumbani kwake Mikocheni leo Mei 4,2024. Kwa mujibu familia hiyo mazishi ya Mkulo aliyewahi pia kuwa Mbunge wa Kilosa mwaka 2005 hadi 2015, zitafanyika kesho Jumapili Mei 5, 2024, Kilosa Morogoro. Marehemu Mkulo pia amewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika miaka ya 1990 hadi alipokwenda kugombea ubunge mwaka 2005.  *Inna lillahi wa inna ilayhi rajioon*

'Elimisheni jamii mabadiliko tabianchi'

Hellen Ngoromera, Dodoma Wakati leo dunia ikisherehekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amewataka waandishi wa habari nchini kuielimisha  jamii kuhusu mabadiliko ya tabianchi. Majaliwa amesema hayo leo Mei 3, 2024 mjini hapa, alipokuwa akifunga kilele cha maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari. "Elimisheni jamii na kuielezea kuhusu mabadiliko ya tabiachi, hivi karibuni tumepata mvua nyingi ambazo zilisababisha madhara kwa wananchi hivyo, ninyi kama waelimisha jamii mna wajibu wa kuwakumbusha kujua wajibu wao kuhusu mabadiliko ya tabianchi," amesema Waziri Mkuu Majaliwa. Amesema ikiwa waandishi  wa habari  wataandika habari hizo kwa kueleza kwa kina kuhusu mabadiliko ya tabianchi itawasaidia  wana jamii kufahamu vizuri hivyo kuepuka athari zake mbalimbali. Majaliwa amewataka pia wana habari kuitangaza nchi na kuijengea taswira chanya kimataifa.  Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu ina...