Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Waziri wa Fedha wa zamani Mustafa Mkulo(77), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa.
Marehemu Mustafa Mkulo, enzi za uhai wake, akijibu maswali bungeni. Picha kwa hisani ya Mtandao. |
Kwa mujibu wa tangazo la familia ya Mkulo shughuli za mazishi zitafanyika nyumbani kwake Mikocheni leo Mei 4,2024.
Kwa mujibu familia hiyo mazishi ya Mkulo aliyewahi pia kuwa Mbunge wa Kilosa mwaka 2005 hadi 2015, zitafanyika kesho Jumapili Mei 5, 2024, Kilosa Morogoro.
Marehemu Mkulo pia amewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika miaka ya 1990 hadi alipokwenda kugombea ubunge mwaka 2005.
*Inna lillahi wa inna ilayhi rajioon*
0 Maoni