Waziri Nape aomba Sh. bilioni 180 za matumizi
Mwandishi Wetu,
Wazara ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, inatarajia kukusanya zaidi Sh. Bilioni 100.7 (100,700,000,000) kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato vya wizara hiyo ikiwemo mauzo ya huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, huku ikiliomba Bunge, kuidhinisha kiasi cha Sh. bilioni 180.9 kwa ajili ya matumizi ya wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.
![]() |
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye akiwasilisha bajeti ya wizara yake bungeni mjini Dodoma leo, Mei 16,2024 |
Wazara ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye ameeleza hayo leo Mei 16, 2024 bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025.
Kwa mujibu wa Waziri Nape, makusanyo mengine ya wizara hiyo kwa ujao wa fedha yatatokana na ada ya usajili wa Magazeti, ada ya mwaka ya magazeti, vitambulisho vya waandishi wa habari na machapisho ya picha, mabango na majarida.
Amesema, mbali na makusanyo hayo, wizara hiyo imeandaa Mpango wa Bajeti wa Mwaka 2024/25 kwa kuzingatia, Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.
Waziri huyo amesema pia kwamba bajeti ya wizara yake imezingatia Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2021/22-2025/26), na hotuba ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.
Kuhusu fedha alizoomba kwa ajili ya matumizi ya wizara yake, Waziri Nape amesema, kati ya fedha hizo, kiasi cha Sh. bilioni 88.9 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, huku Sh. bilioni 142,zikiwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kwamba, katika fedha hizo, Sh. bilioni 117.1, ni fedha za ndani na Sh. bilioni 24.8, ni fedha za nje.
0 Maoni