Hot Posts

6/recent/ticker-posts

CRDB yatajwa orodha benki bora duniani 2024

 -Yatajwa pekee kwa Tanzania

Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com

CRDB imetajwa kuwa benki bora zaidi nchini, iking'ara Afrika Mashariki na kutajwa miongoni mwa benki bora barani Afrika mwaka 2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela

Kwa mujibu wa Mtandao wa Kimataifa Global News, Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha Duniani (IMF), zimeitaja CRDB pia kuwa miongoni mwa benki bora duniani kwa mwaka huu 2024 ukanda wa Afrika.

Kwa mujibu wa mtandao huo uliochapisha habari hizo mapema mwezi huu Mei,2024, kulichoipaisha CRDB kuingia kwenye benki ubora ni uwekezaji wake endelevu wa dola milioni 300 (Tsh 780, bilioni) katika eneo uhifadhi mazingira, kupitia mpango wake wa Kijani Bond.

Kwa ukanda wa Afrika Mashariki, nchini Uganda Centenary Bank imetajwa kuwa mshindi wa ubora, wakati ambapo imeadhimisha mika 40 mwaka uliopita 2023 ikiwa na wateja milioni 2.4 huku ikikua kwa kasi.

Kwa mwaka huu, mshindi kutoka nchini Kenya ni Co-operative Bank, inayotajwa kuwa na ongezeko kubwa la mawakala, mtandao wake ukifikia mawakala 17,000 na  kutajwa kuwa na asilimia 91 ya miamala kupitia mfumo wa kidijitali.

Benki hizo tatu za Afrika Mashariki, CRDB, Centenary na Cooperative, zimo miongoni mwa benki 35 bora zilizoainishwa kwa Bara la Afrika na Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani.

Chapisha Maoni

0 Maoni