Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2025

Wanyama 400 wauawa Mikumi

Picha
 -Kamera kunasa wahalifu Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Hifadhi ya Taifa Mikumi inajipanga ili kuweka  kamera zikazowekwa geti la kuingilia hifadhi hiyo eneo la Kijiji cha Doma, Mikumi Mjini inapoishia hifadhi kwenye barabara Kuu kwenda Iringa, inayopita hifadhini humo, ikielezwa kuwa wastani wa wanyama 400 hufa kwa kugonjwa na gari kila mwaka. Kamishna Augustine Masesa Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Kamishna Augustine Masesa amesema hayo Juni 28/2025 akieleza kuwa hatua hiyo inalenga  kuwanasa madereva watakaowagonga wanyama kwenye eneo la hifadhi na magari yanayovunja sheria kwa kutembea mwendo usioruhusiwa.  Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu hifadhi hiyo, ambapo amesema mradi huo unahitaji takriban shilingi bilioni 2. “Tayari upembuzi yakinifu umefanywa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa (UNDP), tunasubiri pesa tu ipatikane kutekeleza mradi huo kwenye eneo hilo la kilometa 50 inapokatiza b...

Mambo matano ya kipekee usiyoyajua Hifadhi ya Taifa Saadan

Picha
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Licha ya Tanzania kuwa na hifadhi 21 za Taifa zenye vivutio mbalimbali vya utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan imebahatika kuwa na vivutio vya kipekee barani Afrika, hivyo kuitofautisha na nyingine. Hifadhi ya Taifa ya Saadani inayopatikana eneo la mikoa ya Pwani   na Tanga ina mambo matano yanayoelezwa kuitofautisha na nyingine nchini, hata barani Afrika hivyo kuwa ya kipekee. Hifadhi hiyo iliyopo katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani   na wilaya za Handeni na Pangani Mkoa wa Tanga ina ukubwa wa takriban Kilomete za mraba 1,100   na ilianzishwa mwaka 2009. Ofisa Mhifadhi, Utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan, Daud Gordon Akizungumza na wanahabari ndani ya hifadhi hiyo, Ofisa Mhifadhi, anayeongoza kitengo cha utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan, Daud Gordon ameyataja mambo hayo kuwa ni makutano ya Bahari ya Hindi na nyika, uwepo wa mlango bahari wa Mto Wami unaoingia Bahari ya Hindi na mazalia ya kasa wa kijani. Mengine ni wanyama na b...

SANAMU YA BIKIRA MARIA YAONEKANA HIFADHI YA TAIFA SAADAN

Picha
- Maajabu mapya ya kipekee Exuperius Kachenje Sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria (Mariam), anayetajwa na vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu na Qur’an Tukufu (Mariam), ndiye mama wa Yesu Kristo (Nabii Issa bin Mariam), imegundulika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani, ikitajwa kuwa ni maajabu mapya yasiyo ya kawaida kwa watalii ndani na nje ya Tanzania, inayoongeza upekee wa hifadhi hiyo kwa utalii. Mti wa mbuyu wenye sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadan. Picha na Exuperius Kachenje Ofisa Mhifadhi kitengo cha Utalii, Hifadhi ya Taifa Saadani (SANAPA) Daud Gordon amebainisha hayo Juni 26, 2025 akieleza kwamba kivutio hicho kipya ni nyenzo muhimu katika kukuza utalii wa kiimani, hata kuweza kuwa sehemu ya hija kwa waamini, hasa wanaoamini na kumheshimu mama huyo kadiri ya mapokeo ya imani zao,mfano ukiwa Kanisa Katoliki. Gordon amesema kuwa sanamu hiyo ya asili inaonekana katikati ya mti wa mbuyu, eneo la Buyuni  ndani ya hifadhi hiyo,...

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Picha
  -Maajabu mapya ya kipekee Exuperius Kachenje Sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria (Mariam), anayetajwa na vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu na Qur’an Tukufu (Mariam), ndiye mama wa Yesu Kristo (Nabii Issa bin Mariam), imegundulika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani, ikitajwa kuwa ni maajabu mapya yasiyo ya kawaida kwa watalii ndani na nje ya Tanzania, inayoongeza upekee wa hifadhi hiyo kwa utalii. Mti wa mbuyu wenye sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadan. Picha na Exuperius Kachenje Ofisa Mhifadhi kitengo cha uta;ii, Hifadhi ya Taifa Saadani (SANAPA) Daud Gordon amebainisha hayo Juni 26, 2025 akieleza kwamba kivutio hicho kipya ni nyenzo muhimu katika kukuza utalii wa kiimani, hata kuweza kuwa sehemu ya hija kwa waamini, hasa wanaoamini na kumheshimu mama huyo kadiri ya mapokeo ya imani zao,mfano ukiwa Kanisa Katoliki. Gordon amesema kuwa sanamu hiyo ya asili inaonekana katikati ya mti wa mbuyu, eneo la Buyuni  ndani ya h...

Mafanikio ya NHC mageuzi ya makazi Tanzania

Picha
-Yaja kivingine na Nyumba Bond - Fursa mpya kwa wananchi kupata nyumba bora Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limepata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, huku likijidhihirisha kuwa   chombo muhimu katika ajenda ya mageuzi ya miji na maendeleo ya sekta ya makazi Tanzania. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah Chini ya Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, NHC limeongeza wigo utendaji wake kupitia uwekezaji wa kimkakati kwenye sekta ya ardhi na majengo, usimamizi bora wa miradi na uanzishaji wa ushirikiano mpya kati ya sekta ya umma na binafsi. Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah anabainisha hayo, huku akimshukuru Rais Samia Suluhu kwa uamuzi wake wa kuingilia kati na kuikwamua miradi mikubwa kadhaa ya NHC iliyokwama, ambayo sasa imeanza tena baada ya kusimama kwa karibu miaka minane. Hamad aliyekuwa akizungumza na   wahariri wa vyombo mbalimbali v...

Vijana 'Kanda Maalum' Mara kufundishwa ukarimu kwa wageni

Picha
  Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, imeanza kutoa mafunzo maalum kwa vijana wa eneo hilo ya namna ya kuwakarimu na kuhudumia wateja ili waingie katika soko la ajira hasa kuhudumia watalii katika maeneo yanayozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Wilaya Serengeti, Victor Rutonesha akizungumza na wanahabari ofisini kwake.   Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Victor Rutonesha amebainisha hayo alipokuwa akizungumza na wanahabari waliotembelea ofisini kwake kujua namna wanavyoshirikiana na TANAPA katika masuala ya uhifadhi na utalii kwenye eneo laHifahi ya Taifa Serengeti.     Rutonesha amesma mbinu hiyo itasaidia vijana wa Serengeti na Mkoa wote wa Mara kupata ajira kwenye kampuni mbalimbali zinazojihusisha na utalii zikiwamo hoteli na kwenye biashara zao binafsi za nje ya hifadhi. “Tumeamua kuanzisha programu hiyo baada ya kugundua vijana wetu hapa wa...

Bilioni 30 za TANAPA kwa wananchi zapunguza ujangili

Picha
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), limetumia zaidi ya shilingi bilioni 30 kutekeleza miradi ya ujiranii mwema katika vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara, ikitekeleza maombi na mahitaji ya jamii husika. kwenye hifadhi hiyo ya tatu kwa ukubwa nchini. Bweni la wasichana lililojengwa naTANAPA katika moja ya Shule za Sekondari wilayni Serengeti mkoani Mara, kupitia Miradi ya Ushirikiano ya Ujirani Mwema. Picha zote na Exuperius Kachenje) Miradi hiyo ya ujirani mwema (SCIPs) inayotekelezwa na TANAPA, kwenye hifadhi hiyo ya tatu kwa ukubwa nchini,  imetajwa kuwa chachu ya kupunguza vitendo vya ujangili na uingizaji mifugo kwenye hifadhi, ambavyo vilikuwa tishio kwa uhai wa wanyamapori na mazingira yanayowazunguka. Ofisa Uhusiano wa Jamii wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Abed Mwesigwa amebaisha hayo akitaja wanufaika ni Wilaya za Serengeti, Bunda, Tarime, Busega, Bariadi, Itilima, Meatu na Ngorongoro katika mikoa y...

Ngome ya Jeshi la Ujerumani, JWTZ kivutio kipya cha utalii wa ndani Serengeti

Picha
-Watanzania waitwa kutalii Na Exuperius Kachenje,daimatznews@gmail.com Ngome ya Jeshi ya zamani y Jeshi la Ujerumani na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, maarufu kwa Jina la Fort Ikoma iliyopo Hifadhi ya Taifa Serengeti, imetajwa kuwa eneo la kipekee linalovutia watalii ndani ya hifadhi hiyo na tasnia ya utalii nchini likiunganisha historia na asili, huku watanzania wakihimizwa kufanya utalii wa ndani ili kujifunza na kufurahia utajiri wa rasilimali za taifa. Twiga wakijivinjari maeneo ya Fort Ikoma, ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti. Picha zote na Exuperius Kachenje. Ofisa Uhusiano ya Jamii wa Hifadhi ya Taifa Serengeti, Abed Mwesigwa amebainisha hayo ndani ya eneo hilo alipokuwa akieleza kuhusu utajiri wa historia na rasilimali zilizopo ndani ya hifadhi hiyo mbele ya waandishi wa habari waliofanya ziara hifadhini hapo jana. Mwesigwa amesema: “Mtalii yeyote akifika Serengeti bila kutembelea Fort Ikoma atakuwa amekosa kupata utajiri wa historia na asili kwani eneo hilo ndipo asili ...

Waandishi wa Habari wa Afrika wapata mafunzo ya kuandika habari za uhamiaji

Picha
Na Lucy Ngowi, daimatznews@gmail.com NAIROBI - KENYA — WAANDISHI wa Habari kutoka Afrika wamekutana jijini Nairobi kwa ajili ya mafunzo kuhusu mbinu za kuandika habari za uhamiaji. Mafunzo hayo ya siku tatu yameandaliwa chini ya Mpango wa Pamoja wa Uhamiaji wa Wafanyakazi (JLMP) kwa ushirikiano na Tume ya Umoja wa Afrika, IOM, ILO na Shirikisho la Waandishi wa Habari Afrika (FAJ), yakilenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuandika habari za uhamiaji kwa mtazamo wa Kiafrika na kwa kuzingatia ukweli. Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Kanda ya Afrika Mashariki Edwin Righa,  amesesitiza umuhimu wa nafasi ya waandishi wa habari katika kuifanya mitazamo ya umma kuhusu uhamiaji.  “Ninyi ni watafuta ukweli, waandaaji wa ajenda na wanasimulia hadithi kwa niaba ya jamii. Nafasi yenu ni ya kipekee katika jinsi ya kuripoti uhamiaji unaeleweka na kuzungumzwa katika jamii zetu,” amesema. Amesena Bara la Afrika linapitia mabadiliko makubwa ya kiuchumi, huku vijana wengi wakihamia kutoka n...

PPP Center yapika wataalam miradi ya ubia

Picha
- Lengo kupata miradi yenye tija,kuipunguzia mzigo Serikali Mwandishi Wetu, Arusha Kituo cha Ubia kati Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre), kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, kinaendesha mafunzo maalum ya ubobezi wa PPP kwa hatua tatu tofauti. Hatua hizo ni Ngazi ya Msingi, Utayarishaji Miradi na Uendeshaji pamoja na Usimamizi Miradi ya PPP, ili kuwajengea uwezo watumishi katika kuibua na kuchakata miradi ya maendeleo yenye tija kwa utaratibu PPP. Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Miradi wa PPP-Center, Dk. Suleiman Kiula Uendeshaji wa mafunzo hayo ambao ni jukumu la Kisheria la Kituo hicho cha Ubia, yana lengo la kuongeza wataalam zaidi, watakaoweza kutayarisha miradi ya PPP yenye tija kwa ufanisi itakayokuwa kivutio kwa wawekezaji kutoka sekta binafsi ndani na nje ya nchi, hivyo kuipunguzia Serikali mzigo wa bajeti ya maendeleo. Mafunzo hayo kwa Hatua ya Uandaaji Miradi yamefanyika mkoani Arusha kwa siku 10 mapema mwezi huu wa Juni, yakiwajumuisha watendaji kut...