Vijana 'Kanda Maalum' Mara kufundishwa ukarimu kwa wageni
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, imeanza kutoa mafunzo maalum kwa vijana wa eneo hilo ya namna ya kuwakarimu na kuhudumia wateja ili waingie katika soko la ajira hasa kuhudumia watalii katika maeneo yanayozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Serengeti, Victor Rutonesha akizungumza na wanahabari ofisini kwake. |
Kaimu
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Victor Rutonesha amebainisha hayo alipokuwa akizungumza
na wanahabari waliotembelea ofisini kwake kujua namna wanavyoshirikiana na
TANAPA katika masuala ya uhifadhi na utalii kwenye eneo laHifahi ya Taifa
Serengeti.
Rutonesha amesma mbinu hiyo itasaidia vijana wa
Serengeti na Mkoa wote wa Mara kupata ajira kwenye kampuni mbalimbali
zinazojihusisha na utalii zikiwamo hoteli na kwenye biashara zao binafsi za nje
ya hifadhi.
“Tumeamua kuanzisha programu hiyo baada ya
kugundua vijana wetu hapa wamepungukiwa ukarimu, hii ni kwa nia njema tu .
Lakini hili pengine linatokana na mila na desturi za wenyeji wa mkoa huu, zina
upungufu wa ukarimu hasa wanapohudumia wateja hata katika biashaa zao binafsi,”
amesema Rutonesha.
Kwa mujibu wa Rutonesha, wamegundua kuwa wasipofanya
hivyo uwekezaji utakapoanza na kushamiri, utawaacha nje vijana wa mkoa huo
kutokana na sababu mbalimbali, kikubwa kikiwa ni mila, desturi na mazoea ya
wenyeji wa mkoa huo.
“Kwa mfano baadhi ya mila za baadhi ya makabila
ya mkoa huu zinakataza mwanamke kumtuma mwanaume kwa kudhani kwamba amemdharau.
Mwanamke anaweza kwenda dukani au hotelini akamtuma mhudumu wa kiume amletee
soda ainafulani,lakini yule mhudumu akalete soda aina nyingine akaifungua na
kumpa mteja huku akimwambia kunywa hiyo ndio iliyopo, uliyotaka hakuna. Hayo yametokea,
jambo ambalo linawafanya vijana kushindwa kuajirika katika kampuni hasa zinaongozwa
na wanawake,” amesema.
Rutonesha ameongeza: “Vijana wengi wanaishi kwa
mazoea ya tamaduni zao, hawajui umuhimu wa kujali mteja katika biashara zao.
Matokeo ya hali hiyo, vijana wanaofanyakazi kwenye hoteli na kampuni za utalii
wilayani Serengeti wanatoka Kilimanjaro na mikoa mingine.Kwa sababu hiyo, sisi
viongozi hatuwezi kuacha haya yaendelee.”
Amesema wameanza kuwapa elimu vijana na akina
mama wanaozungukwa na Hifadhi ya Taifa erengeti na maeneo mengine kwa sababu
uwekezaji wa mahoteli makubwa na biashara mbalimbali zinaanza kufunguliwa.
Akizungumzia miradi inayotarajiwa kuchochea
fursa za kiuchumi wilayani humo, Kaimu Mkurugenzi Rutonesha amesema kwa sasa
hoteli nyingi za kitalii zitajengwa kwenye vijiji vinavyopakana na hifadhi
ambavyo tayari vina mpango wa matumizi bora ya ardhi.
Ingawa hakutaja idadi ya hoteli zinazotarajiwa
kujengwa maeneo hayo ya vijiji, amesema halmashauri inaendelea kupokea maombi
ya watu wanaotaka kuwekeza hoteli zikiwamo zenye hadhi ya nyota tano na biashaa
nyingine kubwa.
Kaimu Mkurugenzi huyo wahalmashauri amesema
biashara hizo kubwa zitakuwa kwenye maeneo ya wananchi ambao vijiji vyao
vimetenga maeneo ya uwekezaji na utalii kwa ujumla, hivyo wakazi na wenyeji wa
maeneo hayo hawana budi kujiandaa kupokea na kufanya biashara na wageni kwa
lugha ya ukarimu na uaminifu.
Maoni
Chapisha Maoni