Bilioni 30 za TANAPA kwa wananchi zapunguza ujangili
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com
Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), limetumia zaidi ya shilingi bilioni 30 kutekeleza miradi ya ujiranii mwema katika vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara, ikitekeleza maombi na mahitaji ya jamii husika. kwenye hifadhi hiyo ya tatu kwa ukubwa nchini.
Bweni la wasichana lililojengwa naTANAPA katika moja ya Shule za Sekondari wilayni Serengeti mkoani Mara, kupitia Miradi ya Ushirikiano ya Ujirani Mwema. Picha zote na Exuperius Kachenje) |
Miradi hiyo ya ujirani mwema (SCIPs) inayotekelezwa
na TANAPA, kwenye hifadhi hiyo ya tatu kwa ukubwa nchini, imetajwa kuwa chachu ya kupunguza vitendo vya ujangili na uingizaji
mifugo kwenye hifadhi, ambavyo vilikuwa tishio kwa uhai wa wanyamapori na
mazingira yanayowazunguka.
Ofisa Uhusiano wa Jamii wa Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti, Abed Mwesigwa amebaisha hayo akitaja wanufaika ni Wilaya za
Serengeti, Bunda, Tarime, Busega, Bariadi, Itilima, Meatu na Ngorongoro katika
mikoa ya Mara, Arusha na Simiyu.
“Takriban Shilingi bilioni 34 za TANAPA zimetekeleza miradimbalimbali pamoja na miundombinu ya
afya, elimu, maji, barabara na madaraja huku pia wakitekeleza mradi wa matumizi
bora ya ardhi kwa kushirikiana na wadau wengine,”amesema Mwesigwa na kuongeza:
“Katika miradi hiyo,TANAPA kupitia Hifadhi ya Taifa Ngorongoro, imejenga shule, kuchimba mabwawa ya maji kwa ajili ya mifugo, nyumba za madaktari katika baadhi ya zahanati, nyumba za walimu, bweni la wanafunzi wa kike, barabara, madaraja pamoja na ujenzi wa vituo vya askari ili kuvihami vijiji na wanyama wakali katika vijiji jirani na hifadhi.
Mzee John Marwa mkazi wa Kijiji Pake, Rubanda wilayani Serengeti, mkoani Mara akizungumzia mradi wa barabara waliyojengewa na TANAPA. |
Amebainisha kuwa
Hifadhi ya Serengeti imezungukwa na vijiji 248, vikiwa katika wilaya nane za
mikoa mitatu ambayo ni Mara, Arusha na Simiyu.
Mwesigwa ametanabainisha kuwa tayari vijana
katika vijiji hivyo wameanza kupatiwa ajira kwenye kampuni za ulinzi na
uwindaji, ili kuwainua kiuchumi, hivyo kushiriki ulinzi wa raslimali za taifa.
Hata hivyo, amesema TANAPA limeweka masharti
kadhaa ya utoaji miradi hiyo likiwamo linalotaka vijiji vinavyoomba miradi kutokomeza
ujangili na kuacha kuingiza mifugo kwenye hifadhi kwa ajili ya malisho ili
kulinda ikolojia ya Serengeti ili kukidhi vigezo vya kupata miradi ya
maendeleo.Daraja lililojengwa na TANAPA kati ya miradi ya ujirani mwema iliyotekeleza kwenye vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Serengeti
“Kijiji kinachoshiriki vitendo vya ujangili na uingizaji mifugo kwenye hifadhi, hicho kinakosa sifa ya kupewa miradi hiyo. Kutokana na kigezo hicho, wanavijiji wamekuwa wanadhibitiana wenyewe na kupunguza ujangili, hali inayoleta manufaa zaidi kwa hifadhi na wananchi.
“Majangili wanaotoka mbali na maeneo ya hifadhi
hawawezi kutekeleza uhalifu huo bila kushirikiana na wenyeji,”amesema Mwesigwa.
Mzee John Marwa mkazi wa Kijiji Pake, Rubanda wilayani Serengeti anaishukuru TANAPA kwa kuwajengea barabara ya Nyigoti Nyichoka inayopita katika Kijiji chao kuwaunganisha na maeneo mengine, hali inayowarahisishia usafiri na kupunguza gharama za maisha.
“Awali tulilazimika kwenda
hadi Mugumu ili kupata usafiri kwenda Bunda, lakini sasa tunakwenda moja kwa
moja,” amesema Mzee Marwa.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Bokore, Nelson James alikiri Kijiji chake kujengewa zahanati ya kisasa yenye thamani ya zaidi ya
milioni 400 na barabara yenye urefu wa
kilometa 12, ambayo awali ilikuwa haipitiki hasa wakati za masika.
"Sasa tuna uhakika wa kupata huduma saa 24,
zahanati hii ni mkombozi mkubwa kwa wajawazito,” amesema Nyabikwabe Nyerera
mkazi wa Kijiji cha Bokore.
Maoni
Chapisha Maoni