Dk. Kongela awapongeza wafanyakazi NHC

-Mkurugenzi ataja mambo10 atakayosimamia kufikia malengo Joddet Dominic na Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Kibaha, Pwani . Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Sophia Kongela, ame wapongeza wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa mijadala yenye tija. Amesema ameguswa hasa na mjadala kuhusu bajeti ya shirika hilo kwa mwaka 2025/26, inayolenga kuboresha utendaji kupitia miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa nyumba. Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)Dk.Sophia Kongela, akizungumza wakati akifunga Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC,Kibaha Pwani,Februari 25,2025 . Dk. Kongela ametoa kauli hiyo katika hotuba yake ya kufunga Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NHC uliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kibaha Pwani, Februari 24 na 25, 2025 ambapo a liwahimiza wafanyakazi wa shirika hilo kuendelea kuwa wabunifu, waaminifu, na kujituma katika majukumu y...