Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2025

Dk. Kongela awapongeza wafanyakazi NHC

Picha
-Mkurugenzi ataja mambo10 atakayosimamia kufikia malengo Joddet Dominic na Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Kibaha, Pwani .  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Sophia Kongela, ame wapongeza wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa mijadala yenye tija. Amesema ameguswa hasa na mjadala kuhusu bajeti ya shirika hilo kwa mwaka 2025/26, inayolenga kuboresha utendaji kupitia miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa nyumba. Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)Dk.Sophia Kongela, akizungumza wakati akifunga Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC,Kibaha Pwani,Februari 25,2025 .   Dk. Kongela ametoa kauli hiyo katika hotuba yake ya kufunga  Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NHC uliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kibaha Pwani, Februari 24 na 25, 2025 ambapo a liwahimiza wafanyakazi wa shirika hilo kuendelea kuwa wabunifu, waaminifu, na kujituma katika majukumu y...

Msajili Hazina ataka kasi zaidi NHC, akionya majungu

Picha
-Awaambia NO uteuzi kwa majungu Exuperius Kachenjea na Joddet Dominic, daimatznews@gmail.com Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu amesema Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lina jukumu kubwa katika kutekeleza mageuzi ya sekta ya makazi nchini akihimiza kuongeza ufanisi, kufanya maamuzi kwa haraka na kuhakikisha mali za umma zinatumika ipasavyo. Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), linalofanyika ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Kibaha, mkoani Pwani Februari 24,2025. Mchechu pia amesema mafanikio ya mageuzi hayo yanahitaji mshikamano na uwajibikaji wa pamoja kwa wafanyakazi wote, huku akionya watumishi kuacha majungu badala yake kuchapakazi kwani ndiyo njia ya mafanikio. "Ili tufanikiwe, tunahitaji kuwa na timu inayofanya kazi kwa upendo, siyo kwa majungu. Mimi mwenyewe ninaweza kuwa mmoja wa waathirika wa majungu, lakini nawaombeni sana mfanye kazi kw...

Mshtakiwa dawa za kulevya adai kuitilia shaka Jamhuri

Picha
 -Ni kwa kutotajwa vielelezo vilivyochukuliwa nyumbanil kwake  MwandishiWetu,daimatznews@gmail.com MSHTAKIWA katika kesi ya dawa za kulevya, Sharifa Majani amesema anautilia  shaka upande wa Jamhuri, kwani haukutaja mahakamani vielelezo vilivyochukuliwa nyumbani kwake, ikiwemo hati ya nyumba, kadi za Benki na simu zake. Shughuli za Mahakama ya Mafisadi zikiendelea katika moja ya kesi zilizowahi kusikilizwa na mahakama hiyo.   Mshtakiwa huyo amekana kujipatia nyumba yenye thamani ya Sh milioni 168 kwa kujihusisha na  biashara ya dawa za kulevya. Mshtakiwa huyo wa kwanza alidai hayo Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya wakati akisomewa mashtaka na maelezo ya awali. "Mheshimiwa hapa kuna ukakasi, vielelezo vilivyochukuliwa ndani kwangu upande wa Jamhuri hawakuvisema, hati ya nyumba, simu na kadi za Benki,"alidai mshtakiwa. Sharifa alikana kuwaelezea Polisi kwamba dawa za kulevya zingine zilisafirishwa kwa kut...

Kesi ya 'Mkurugenzi' wa NIC yaelekea patamu

Picha
-Ni ya kuchepusha Sh, Bilioni 1.8  -Mashahidi 119 kutoa ushahidi Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Kesi ya kuchepusha shilingi bilioni1.8 inayo yomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Shirika la Bima la Taifa (NIC), Sam Kamanga na wenzake wawili inaelekea patamu, baada ya mahakama kuelezwa kuwa mashahidi 119 na vielelezo 200 vinatarajiwa kutolewa kuthibitisha mashtaka hayo na upande wa Jamhuri. Mfano wa noti  za Shilingi Elfu Kumi (10,000/=) za Benki Kuu  ya Tanzania Ushahidi huo unatarajiwa kutolewa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya. Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Karen Mrango akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Edgar Bantulaki, umeeleza hayo leo Februari 18, 2025 mahakamani hapo . Wakili Bantulaki aliwataja washtakiwa katika shauri hilo kuwa ni Kamanga, Tabu Selemani na Peter Nzunda ambao wanadaiwa kati ya Mwaka 2013 na 2018 waliongoza...

80% muziki wa kitanzania kusikia viwanja vya ndege Tx

Picha
Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Hamis Mwinjuma na Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile, wameshuhudia utiaji saini makubaliano ya matumizi ya asilimia 80 ya muziki wa wasanii wa kitanzania, kupigwa katika viwanja vya ndege nchini, ili kuwawezesha kufaidi matunda ya kazi zao yatokanayo na malipo ya mirabaha.   Naibu Waziri wa Sanaa,Michezo na Utamaduni,(Kulia) na   Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile, (kushoto) wakishuhudia utiaji saini mikataba itakayowezesha muziki wa Kiswahili kupigwa viwanya vya ndege.katikahfla iliyofanyika hivi karibuni Makubaliano hayo yamesainiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa na Msimamizi wa Haki Miliki (COSOTA) Doreen Sinare, na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA)  Abdul Mombokaleo, ambapo katika makubaliano hayo, imependekezwa muziki wa wasanii wa kitanzania kusikilizwa zaidi, lengo likiwa ni kulinda kazi za sanaa za watanzania pamoja na kuutangaza...

Ommy Dimpoz azindua Tuzo za Komedi Tanzania, kutolewa Februari 14

Picha
Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Msanii Maarufu wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz, amezindua Tuzo za Komedi Tanzania (TCA), zinazojulikana kama 'Tanzania Comedy Awards', zinazotarajiwa kutolewa Februari 14, mwaka huu. MsaniiOmmy Dimpozakizungumza wakati wa kutangaza tuzo hizo   Hafla yautangazaji tuzo hizo imefanyiks katika Ukumbi wa Superdom Masaki, jijini Dar es Salaam, zikihusisha wasanii wote wa uchekeshaji nchini. Kaimu Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Dk. Gervas Kasiga, ametangaza vipengele 17 vya tuzo hizo, ambapo washindi wa tuzo tatu kubwa watajinyakulia zawadi za fedha kama ifuatavyo: - Mchekeshaji Bora wa Kike atapewa zawadi ya Sh20 milioni - Mchekeshaji Bora wa Kiume atanyakua Sh20 milioni - Mchekeshaji Bora wa Mwaka atabeba Sh30 milioni Washindi wa vipengele vingine vya tuzo hizo watapata zawadi ya Sh milioni 5 kila mmoja. Hafla ya uzinduzi wa tuzo hizo ilifanyika usiku wa kuamkia Januari 16, 2025, katika Ukumbi wa Johari Rotana, jijini Dar es Salaam.  

Kama unamtaka Shilole, 'mfuate Mafuta ya Korie'

Picha
Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Msanii na mfanyabiashara Zuwena Mohammed maarufu  Shilole , ametangazwa kuwa Balozi wa  Mafuta ya Kupikia Korie , katika kilichoelezwa ni kuongeza mvuto wake kwa chapa hiyo iliyoboreshwa kwa mwonekano mpya na vifungashio vipya Msanii Shilole(Katikati), akiongea baada ya kutambulishwa kuwa Balozi wa Mafuta ya Kupikia ya Korie  jijini Dar es Salaam. Shilole aliongoza uzinduzi wa vifungashio vya  nusu lita na robo lita  vya mafuta ya Korie, hatua inayolenga kuwafanya Watanzania wengi zaidi kupata mafuta hayo ya kupikia yenye ubora kwa urahisi. Akizungumza wakati wa hafla hiyo kubwa, Shilole alionyesha furaha yake na kusema: "Korie Kipochi kimefika kwa mikono sahihi na kwa wakati sahihi! Hata unapomaliza mafuta ghafla, Korie Kipochi ni suluhisho la haraka—kamili kwa dharura za jikoni." Vifungashio hivi vipya, vilivyotengenezwa kwa mifuko laini ya plastiki chini ya jina  "Kipochi" , vimebuniwa kwa bei nafuu ili kuwafik...

Mnigeria wa dawa za kulevya waachiwa huru

Picha
 DPP asema hana nia kuendeleza kesi  Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com MKURUGENZI wa Mashtaka Nchini (DPP) ameiomba Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imwachie huru raia wa Nigeria Emmanuel Chiabo na mwenzake wanaoshtakiwa kwa kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine Kilogramu 29.71 sababu hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Mahakama mbele ya Jaji Godfrey Isaya imepokea maombi hayo na kukubali kuondoa shtaka dhidi ya Chiabo na Goodness Remy. Wakili wa Serikali Glory Kilawe akiwakilisha Jamhuri aliwataja washtakiwa kuwa ni Chiabo na Goodness Remy ambao walishtakiwa kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine. "Mheshimiwa shauri lilikuja kwa ajili ya kuwasomea washtakiwa mashtaka na usikilizwaji wa awali lakini Jamhuri tunaomba kuondoka shtaka chini ya kifungu namba 91(1) Cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022,"alidai. Alidai kuwa washtakiwa wanadaiwa Aprili 19 mwaka 2023 maeneo ...

'Kocha wa makipa Simba', wenzake wakana mashtaka dawa zakulevya

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MSHTAKIWA Saidi Matwiko na mkewe Sarah Joseph wamekana kukutwa na dawa za kulevya wakati upekuzi ulipofanyika nyumbani kwao Kivule katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam. Matwiko na Sarah wamekana maelezo hayo waliposomewa mashtaka na maelezo ya awali katika mashtaka yanayowakabili ya kusafirisha dawa za kulevya na wenzao wanne pamoja na  aliyekuwa Kocha wa Makipa wa Timu ya Simba Muharami Sultani. Kesi hiyo imeanza kusikilizwa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu mbele ya Jaji Godfrey Isaya  Februari 5,2025. Watuhumiwa hao wanashtakiwa wakidaiwa kuongoza genge la uhalifu, kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine kilo 34.89. Pia mmiliki wa Ktuo cha Michezo cha Cambianso, kilichoko Tuangoma, Kigamboni mkoani Dar es Salaam, Kambi Zubery anashtajiwa kwa kutakatisha fedha ambapo anadaiwa kujipatia magari matano aina ya Tata huku akijua Mali hiyo inatokana na zao la kuongoza genge la Uhalifu.  Akiwasomea mashtaka watuhum...