Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com
Msanii Maarufu wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz, amezindua Tuzo za Komedi Tanzania (TCA), zinazojulikana kama 'Tanzania Comedy Awards', zinazotarajiwa kutolewa Februari 14, mwaka huu.
![]() |
MsaniiOmmy Dimpozakizungumza wakati wa kutangaza tuzo hizo |
Hafla yautangazaji tuzo hizo imefanyiks katika Ukumbi wa Superdom Masaki, jijini Dar es Salaam, zikihusisha wasanii wote wa uchekeshaji nchini.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Dk. Gervas Kasiga, ametangaza vipengele 17 vya tuzo hizo, ambapo washindi wa tuzo tatu kubwa watajinyakulia zawadi za fedha kama ifuatavyo:
- Mchekeshaji Bora wa Kike atapewa zawadi ya Sh20 milioni
- Mchekeshaji Bora wa Kiume atanyakua Sh20 milioni
- Mchekeshaji Bora wa Mwaka atabeba Sh30 milioni
Washindi wa vipengele vingine vya tuzo hizo watapata zawadi ya Sh milioni 5 kila mmoja.
Hafla ya uzinduzi wa tuzo hizo ilifanyika usiku wa kuamkia Januari 16, 2025, katika Ukumbi wa Johari Rotana, jijini Dar es Salaam.
0 Maoni