Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Kesi ya 'Mkurugenzi' wa NIC yaelekea patamu

-Ni ya kuchepusha Sh, Bilioni 1.8 

-Mashahidi 119 kutoa ushahidi

Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Kesi ya kuchepusha shilingi bilioni1.8 inayoyomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Shirika la Bima la Taifa (NIC), Sam Kamanga na wenzake wawili inaelekea patamu, baada ya mahakama kuelezwa kuwa mashahidi 119 na vielelezo 200 vinatarajiwa kutolewa kuthibitisha mashtaka hayo na upande wa Jamhuri.

Mfano wa noti  za Shilingi Elfu Kumi (10,000/=) za Benki Kuu  ya Tanzania

Ushahidi huo unatarajiwa kutolewa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Karen Mrango akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Edgar Bantulaki, umeeleza hayo leo Februari 18, 2025 mahakamani hapo .

Wakili Bantulaki aliwataja washtakiwa katika shauri hilo kuwa ni Kamanga, Tabu Selemani na Peter Nzunda ambao wanadaiwa kati ya Mwaka 2013 na 2018 waliongoza genge la Uhalifu maeneo tofauti tofauti Dar es Salaam, Rukwa, Kilimanjaro, Arusha , Mbeya, Morogoro na Kigoma.

Inadaiwa kwa nyakati tofauti kwa njia ya ulaghai walijipatia Sh 1,863,017,400.75 kutoka Shirika la Taifa la Bima.

Washtakiwa wanadaiwa walijipatia fedha hizo kwa kughushi hundi  na mshtakiwa wa nne Nzunda anadaiwa kwa kutumia fedha hizo alinunua mashamba matano maeneo tofauti tofauti.

Washtakiwa waliposomewa maelezo ya awali walikana kuhusika kuchepusha fedha hizo.

Walidai wanafahamu kulikuwa na fedha zilizochepushwa lakini hawakuhusika.

Washtakiwa walikana kusababisha hasara ya kiasi hicho cha fedha na walikana pia kushirikiana na maafisa wa Benki kutenda kosa hilo.

 Kamanga alikana Kuzuia ukaguzi kufanyika na kwamba wizi ulifanyika ndani ya miaka minne bila kubainika na Wakuu wa idara.

Mshtakiwa Tabu alidai kwa nafasi yake ya uhasibu alifanya uchunguzi wake mwenyewe na kugundua fedha zilichepushwa na alitoa ripoti ya fedha hizo.

Tabu alidai Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alikuwa anafanya ukaguzi kila mwaka lakini hakumbuki kama uliwahi kufanyika ukaguzi maalum katika Shirika la Taifa la Bima.

Walishtakiwa walikana kujipatia fedha hizo kwa kughushi hundi  na mshtakiwa Nzunda alikana kutumia fedha hizo kununua mashamba matano maeneo tofauti tofauti na garu huku akijua ni mazalia ya Makosa ya jinai.

Chapisha Maoni

0 Maoni