Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2024

NEEC 'yawafunda' wanawake, vijana

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com KATIBU Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), BengI Issa, amewataka wanawake na vijana kutumia vizuri na kwa nidhamu fedha zinazotolewa na taasisi za uwezeshaji, ili kasi ya kujikwamua kiuchumi iongezeke na kuleta matokeo chanya kwa fedha zinazopelekwa. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake  na Vijana wa Kanisa la TAG City Light Temple, Goba, Dar es Salaam, Issa amesema Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan ina nia nzuri na wazi ya kuwawezesha Watanzania kiuchumi kwa kutoa mitaji wezeshi, hasa kwa makundi maalumu kwa kutumia majukwa ya uwezeshaji.  Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), BengI Issa, (kulia) akimkabidhi Taulo za Kike mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Matosa  katika hafla  ya uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake na Vijana wa Kanisa la TAG City Light Temple, iliyofanyika jana Januari 30, 2024   Goba,  j...

Serikali yajidhatiti kukabili athari za kimazingira

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wizara za kisekta, imeanza kufanya tathmini nchi nzima ili kubainisha maeneo yanayohitaji kufanyiwa maboresho kukabiliana na athari za kimazingira. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)  Dk. Selemani Jafo amebainisha hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe, Khalifa Mohammed Issa aliyetaka kujua lini Serikali itafanya utafiti kubaini maeneo yaliyoathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na kuchukua hatua. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Selemani Jafo akijibu maswali bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu katika Kikao cha Pili, Mkutano wa 14 wa Bunge jijini Dodoma leo Januari 31/2024 . Akijibu swali hilo, Dk. Jafo amesema katika kushughulikia changamoto ya mabadiliko ya tabianchi Serikali imeanza kuyafanyia kazi maeneo hayo kwa kutekeleza miradi ya mazingira pande zote mbili za Muungano. "Ofisi ya Makamu wa Rai...

Serikali yaleta kanuni kusimamia maeneo nyeti

Picha
  -Yalenga kupunguza mgongano ya wanyamapori na wananchi -Yatoa kipaumbele maeneo 12 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Serikali   imeanza kuandaa Kanuni za Kutangaza na Kusimamia Maeneo 77 Nyeti na Lindwa yaliyoainishwa, inayotarajiwa kukamilika kabla ya Juni, 2024, ikiwa pia katika hatua ya kupunguza mgongano wa matumizi ya rasilimali kati ya wanyamapori na wananchi. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Selemani Jafo amebainisha hayo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma Januari 24, 2024. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Selemani Jafo, akizungumza mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya maji na Mazingira Januari 24,2024, jijini Dodoma.   Amesema Serikali imeyapa kipaumbele maeneo 12 kwa ajili ya kufanyiwa tathmini zaidi kwa kuzingatia umuhimu wake kiikolojia kutokana na uharibifu wa mazingira. ā€œTupo katika hatua za kupunguza mgongano wa matumizi ya rasilimali kat...

Balozi Nchimbi avaa namba 11 Ukatibu Mkuu CCM

Picha
-Makomredi 10 wamtangulia -WanaCCM matumaini mapya Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Hahika siku hazigandi, Balozi Emmanuel Nchimbi (52), ametangazwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa CCM leo Januari 15,2024 ikiwa zimetimia saa 1,200 sawa na siku 50, tangu kujiuzulu kwa Daniel Chongolo katika wadhifa huo Novemba 2023. Mapema leo akili, macho na masikio ya wanaCCM yalielekezwa Zanzibar, kusubiri mrithi wa nafasi hiyo nyeti ya utendaji ndani ya CCM. Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan (kushoto), akimpongeza Katibu Mkuu wa mpya wa CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi, baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho mjini Unguja Januari 15, 2024. Wapo pia ambao pamoja na akili na masikio yao, viroho viliwadunda, wakitamani na kusubiri huenda wakatajwa kurithi nafasi hiyo nyeti na kuweka historia mpya ya chama hicho cha siasa kikongwe Tanzania na Afrika, baada ya kukamilika kwa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM(NEC), uliofanyika leo. Lakini, taarifa iliyotolewa na CCM kupitia ...

Mkapa ataka maofisa biashara kubadilika

Picha
- Ataka watimize majukumu kwa ufanisi -Ni katika idara mpya Biashara Viwanda na Uwekezaji Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Maofisa Biashara nchini wametakiwa kutumia elimu   waliyoipata kubadilisha mitizamo yao na kutekeleza majukumu  ya idara yao mpya ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji kwa ufanisi.          Mkurugenzi wa Leseni wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Andrew Mkapa, ametoa wito huo wakati akifunga mafunzo ya Maofisa Biashara  kuhusu  Sheria ya Leseni za Biashara na Viwanda, yaliyofanyika kwa  siku nne mkoani Singida.        Mkurugenzi wa Leseni wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Andrew Mkapa, akizungumza katika mafunzo ya maofisa biashara mkoani Singida, Januari 12,2024 . "Mafunzo haya yasiishie hapa, tuendelee kuwasiliana hata busara ikatawale zaidi katika kuwasilisha namna ya kuleta mabadiliko katika utekelezaji wa majukumu kwa ufanisi," amesema Mkapa na kuo...

Othman wa ACT kutikisa mikoa mitano

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Zanzibar, Othman Masoud Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar atafanya ziara ya kuimarisha chama hicho katika mikoa mitano ya Tanzania Bara. Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Zanzibar, Othman Masoud Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar katika moja ya mikutano yake ya kisiasa. Makamu huyo wa Kwanza wa Rais, atafanya ziara hiyo kuanzia Januari 14 hadi 21 katika mikoa ya Ruvuma, Mkoa wa Kichama Selous, Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es salaam. Taarifa ya ACT Wazalendo imesema kwenye ziara hiyo, Othman Masoud atazungumza na viongozi wa majimbo yote kwenye mikoa hiyo mitano kupitia mikutano mikuu ya mikoa na kufanya shughuli nyingine za kisiasa.

RC aonya maofisa biashara rushwa

Picha
- Awataka kupunguza kero kwa wananchi -Mkurugenzi BRELA awataka kubadili mtazamo Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Maofisa Biashara nchini, wameonywa wakitakiwa kuepuka rushwa, badala yake kutoa elimu kwa wananchi sanjari na kupunguza kero zinazojitokeza, ikiwemo gharama zisizo halali za urasimishaji biashara. Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter  Serukamba leo Januari 9, 2024 wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Maofisa Biashara kutoka mikoa ya Dodoma, Singida, Rukwa, Simiyu, Katavi na Tanga, yanayofanyika  mkoani Singida.  "Nitoe rai kwenu, mjiepushe na vishawishi vya kuomba au kupokea rushwa katika utoaji huduma zenu, mafunzo haya yakawezeshe kutoa huduma saidizi kwa wananchi kwa weledi na uaminifu,  ili yakaonyeshe matokeo chanya kama ilivyokusudiwa na Serikali," amesema Serukamba. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akifungua mafunzo ya Maofisa Biashara wa mikoa sita ya Tanzania Bara mkoani Singida leo Januari 9,2024.....

Rostam sasa atua Mombasa

Picha
-Awekeza trilioni 4 Dongo Kundu -Ni katika gesi asilia, apambana na bilionea wa Mombasa  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Bilionea Mtanzania, Rostam Aziz,  ameanza ujenzi wa kituo cha gesi asilia ya kupikia (LPG) na eneo la kuhifadhia gesi hiyo katika mji wa Mombasa nchini Kenya, wenye thamani Dola za Marekani bilioni 1.9 sawa na takriban shilingi trilioni 4.55. Taarifa zinaeleza kuwa, mradi huo ni mwendelezo wa Kampuni ya Taifa Gas inayomilikiwa na Rostam (pichani chini) , kutanua wigo wa shughuli zake katika nchi nyingine za Afrika Mashariki na kusini, mbali na Tanzania. Mwenyekiti wa Kampuni za Taifa Group,   Rostam Aziz Tayari mwaka 2023, Rostam ametangaza kufanya uwekezaji uwekezaji mpya, nchini Zambia unaofikia kiasi cha Dola za Marekani milioni 100 katika sekta ya nishati na madini ambazo ni sawa na takriban shilingi bilioni 250 kupitia Taifa Gas. Uwekezaji wa sasa nchini Kenya, unatajwa pia kumuweka Rostam katika ushindani wa kibiashara na Mohamed Jaffer anay...