Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2023

TTCL yaipa 'tano' DCPC

Picha
 Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), limeipongeza Klabu Waandishi wa Habari Dar es Salaam (DCPC) kwa ushirikiano wa kikazi na kimkakati, iliouonyesha kwa shirika hilo kipindi chote cha mwaka 2023. Pongezi hizo zimetolewa leo Desemba 29, 2023 na Mkurugenzi wa TTCL, Mhandisi Peter Ulanga kupitia kwa maofisa uhusiano wa shirika hilo, Adeline Berchimance na Rehema Nyangasa waliotembelea ofisi za DCPC Mtaa wa Samora, ambapo wamewasilisha zawadi na ujumbe maalum kutoka kwa Mhandisi Ulanga, aliyesema klabu hiyo imefanya vizuri katika kuandika habari za shirika hilo na kulitangaza.  Ofisa Uhusiano wa TTCL, Adeline Berchimance(Kushoto), akikabidhi zawadi maalum kwa Katibu Mkuu wa DCPC, Fatma Jalala(Kulia) pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji DCPC Bakari Matutu. Mwingine kushoto ni Rehema Nyangasa ambaye pia  ni Ofisa Uhusiano wa TTCL, wakati ujumbe wa kampuni hiyo ulipotembelea ofisi za DCPC, Mtaa wa Samora, Dar es Salaam Desemba 29, 2023...

Wizara kuanzisha maduka ya ardhi

Picha
 - Yatakuwa kwenye ofisi zake -Waziri aagiza mkurugenzi kusimamishwa kazi -Ataka waliomilikishwa maeneo ya wazi kujisalimisha -Ni katika siku 100 akiwa ofisini Exuperius Kachenje, daimatz@gmail.com Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amesema wizara hiyo itaanzisha maduka ya ardhi katika ofisi zake na wilaya na mikoa. Amesema, lengo la hatua hiyo ni kukoa wananchi dhidi ya udanganyifu unaofanyika kwenye ununuzi wa ardhi maeneo mbalimbali kwa sasa. Akizungumza katika kikao kazi na Wahariri wa vyombo vya Habari nchini kupitia, Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), kuhusu siku 100 tangu alipoingia kuiongoa wizara hiyo Dar es Salaam leo Desemba 22, 2023 Waziri Silaa amebainisha hayo. Waziri Silaa ametangaza kupiga marufuku mauziano holela ya ardhi ambazo hazijapangwa kuanzia sasa, akipiga marufuku pia wenyeviti wa mitaa kujihusisha na uuzaji ardhi. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa "Tunazo takwimu zinaonyesha kuna kampuni binafsi mbaya...

Papa Fransisko atangaza Mafinga Jimbo jipya Katoliki

Picha
  Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Fransisko, ameongeza eneo la utawala ndani ya kanisa hilo Tanzania, kwa kutangaza Jimbo jipya Katoliki la Mufindi, huku akimteua Padre Vincent Cosmas Mwagala (pichani chini) kuwa askofu wa kwanza wa jimbo hilo. Askofu Mteule Cosmas Mwagala wa Jimbo Katoliki la Mufindi Taarifa ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), iliyotolewa leo Desemba 22 na kusainiwa na Katibu Mkuu wake, Padre Charles Kitima imeeleza hayo, ikimtaja Askofu Mteule Mwagala mwenye umri wa miaka 50 kuwa ni mzaliwa wa Makungu wilayani Mufindi katika Jimbo Katoliki la Iringa. Zaidi soma taarifa ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) chini;  

BRELA, TAKUKURU 'zafunga ndoa' kukabili rushwa

Picha
  - BRELA yapokea barua 120 za    TAKUKURU kwa mwezi -Ni zinazohitaji taarifa za kampuni -Zimo za kuwaita maofisa BRELA mahakamani   Exuperius Kachenje, daimatz@gmail.com Wakati mwaka 2023 ukielekea ukingoni Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imeongeza kasi katika utendaji wake, ikilenga kuboresha utendaji na utoaji huduma zake kwa wananchi, lakini zaidi safari hii ikilenga kukuza ushirikiano kiutendaji kunakoondoa maswali kuhusu taarifa za usajili wa kampuni mbalimbali.   Hii ni kutokana na ukweli kwamba kila mwezi BRELA hupokea takriban barua 120 kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) zinazohitaji taarifa za usajili wa kampuni, lakini pia maofisa wa BRELA wamekuwa wakiitwa mara kwa mara TAKUKURU kwa ajili ya mahojiano kuhusu masuala yanayohusu usajili wa kampuni.     Ukweli huo wa BRELA kupokea barua kwa wingi kutoka TAKUKURU zikihtaji taarifa za usajili wa kampuni mbalimbali kuiwezesha mamlaka hiyo ya Seri...

Rais Samia atangaza Kinu cha kwanza Bwawa la Nyerere kuwashwa 'siku14 zijazo

 Mwandishi Wetu,daimatz@gmail.com Ikulu ya Rais Samia Suluhu Hassan, imetangaza kuwa kinu cha kwanza cha kuzalisha umeme katika Bwawa la Mwalimu Nyerere, kitawashwa Januari 2024, ikiwa ni takriban siku 14 kuanzia leo. Tangazo hilo la Ikulu limekuja huku maeneo mbalimbali ya Tanzania yakikabiliwa na mgawo wa umeme, hali inayotajwa kiuchangia kushuka kwa uzalishaji. Hata hivyo, Bwawa hilo la Mwalimu Nyerere linatarajiwa kumaliza tatizo la upungufu wa umeme nchini kwa kuzalisha megawat 2100, litakapokamilika. Katika taarifa yake, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu,  Zuhura Yunus leo Desemba 18,2024, amemnukuu Rais Samia akieleza;  " Serikali inatarajia kuwashwa kinu cha kwanza cha kufua umeme mwezi Januari, 2024 katika bwawa la Nyerere, ikiwa ni jitihada za kuzalisha umeme wa kutosha ambao ni muhimu kwa wazalishaji." Rais ameeleza hayo katika hafla ya utoaji Tuzo za Rais kwa wazalishaji bora, (PMAYA) jijini Dar es Salaam, ambapo amewataka wazalishaji wa bidhaa kupitia ...

RAIS SAMIA 'ATANGULIZA ZAWADI' KUAGA 2023

Picha
- Aanza panga pangua viongozi - Agusa 24 wamo MaDc, Wakurugenzi wa halmashauri, makatibu tawala - Ateua, atengua, MaRC, Mawaziri joto lapanda Mwandishi Wetu, daimatza@gmail.com Siku, saa na dakika zinazidi kukatika kuelekea sikukuu ya Krismas inayoendana na kumalizika kwa mwaka 2023, ambayo huambatana na kutumiana salam za kutakiana heri na kupeana zawadi, ikiwa ni sehemu ya desturi ya maisha ya Watanzania. Wakati sikukuu hizo zikisubiriwa, leo Desemba 14, 2023, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko yanayowagusa watendaji 24 katika ngazi ya mikoa, wilaya na halmashauri nchini. Hatua hiyo ya Rais Dk. Samia inaweza kutafsiriwa kama 'ametanguliza zawadi' ya sikukuu kwa walioguswa, ikizingatiwa kwamba umefanyika siku 13 kabla ya kusherehekea Krisimas na siku 20, kabla ya kuhitimisha mwaka 2023 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2024, ikikumbukwa kwamba, 'zawadi ni zawadi'. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan Taarifa ya Ikulu kupitia kwa M...