Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2025

Samia asamehe 1,036

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara,leo Desemba 9,2025, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ametangaza msamaha kwa wafungwa 1036 walio katika magereza mbalimbali nchini. Rais Dk.Samia Suluhu Hassan Msamaha huo unawagusa wafungwa wenye makosa mbalimbali walioonyesha tabia njema. Zaidi soma taarifa kamili hapa chini;   

Saa wakurugenzi mashirika ya umma zahesabika

Picha
  -Serikali yaja na mageuzi ya sheria -Wana takriban siku 200 kubaki madarakani -Mageuzi kugusa mamlaka ya Rais kuwateua -Mashirika kusajili hisa, kuongeza wajibikaji Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Siku za wakurugenzi wa mashirika ya umma na wakala za Serikali nchini zinahesabika, wakibakiwa na takriban siku 217 kabla ya kujua hatma yao, iwapo watasalia au kuondoka kwenye nafasi hizo. Kuanzia Desemba 2025, siku hizo 217 sawa na wastani wa miezi saba, zikizidishwa kwa saa 24 za kila siku moja, zinakuwa jumla ya saa 5,208 , muda unaolingana na kipindi kilichosalia kabla ya kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa ajira. Profesa Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji Hatua hiyoi inakuja baada ya Serikali kutangaza mpango wa kufanya mageuzi makubwa katika uongozi wa mashirika ya umma, unaotarajiwa kuanza rasmi Julai 1, 2026 Kwa mujibu wa Serikali, mabadiliko hayo yatakwenda na mabadiliko ya sheria ambapo Wakurugenzi wa mashirika watalazimika kuo...

Masharti 5 kwa Polisi kukamata raia sasa ni haya

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene, ameagiza Jeshi la Polisi nchini kuhakikisha kuwa ukamataji wa watu unafanywa kwa kuzingatia sheria, ustaarabu na maadili ya kazi ya polisi.  Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam, Desemba 8, 2025, akimwelekeza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Camillus Wambura, kusitisha mara moja vitendo vya ukamataji wa mabavu vinavyofanywa kwa askari waliovaa kama "ninja", wasio na sare na wakiwa na silaha nzito. Akiweka maelekezo hayo hadharani, Waziri Simbachawene amelikumbusha Jeshi la Polisi  masharti matano muhimu ya ukamataji unaokubalika kisheria na unaoakisi staha ambayo ni pamoja na; 1.  Askari kuvaa sare rasmi za Polisi Waziri Simbachawene amekataza ukamataji unaofanywa na askari waliovaa mavazi kama ninja au nguo zisizowatambulisha kama polisi. Sare ni utambulisho wa kisheria na chanzo cha uaminifu kwa wananchi. 2. Ukamataji ufanyike kwa kutambuli...

NHC na safari ya miaka 64 ya Uhuru, miaka 63 ya kujenga makazi bora

Picha
- Ni shirika lililoanzishwa na Mwalimu Nyerere linabeba ndoto ya makazi ya kisasa kwa kila Mtanzania -Miradi ya ubia, fedha, teknolojia vyabeba mwelekeo mpya NHC Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tanganyika, sasa Tanzania Bara ilipata Uhuru wake tarehe 9 Desemba 1961. Leo, tarehe 9 Desemba 2025, taifa linatimiza miaka 64 tangu kuanza kwa safari yake ya kujitawala. Rais wa Kwanza wa Tanzania na Baba wa Taifa,Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere(Katikati), akikagua ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi zilizojengwa na NHC, eneo la Magomeni miaka ya 70. (Picha ya Maktaba) Pamoja na ushindi huo wa kihistoria, wakoloni walipoondoka hawakuacha mpango wowote wa makazi bora kwa Tanganyika huru. Ni katika mazingira hayo ambapo Serikali ya Tanganyika chini ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ilitambua kwamba makazi ni hitaji la msingi la binadamu. Mwaka mmoja tu baada ya Uhuru mnamo 1962, Serikali iliunda Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia Sheria ya Bunge Na. 45, i...