TAKUKURU YAWATEGA WALAJI, WATOA RUSHWA UCHAGUZI MKUU

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kigoma imesema kuwa  ina vyanzo vipya vya kupata taarifa na mbinu za kisasa, itakazozitumia kudhibiti vitendo vya rushwa katika hatua mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu katika mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Ofisa Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU Mkoa Kigoma, Abecha Bakari katika kikao kazi na waandishi wa Habari, kuweka mkakati wa pamoja wa ushirikiano katika kufanya kazi wakati wa Uchaguzi Mkuu.

“Pamoja na mambo mengine, pia tumeongeza vyanzo vya taarifa na namna ya kupata taarifa hizo, lakini pia na namna ya  kuzifanyia kazi, hivyo tuna uhakika kuwa mwaka huu udhibiti wa vitendo vya utoaji na upokeaji rushwa utadhibitiwa,” amesema Bakari.

Naye Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa Kigoma, John Mgallah aliomba ushirikiano kutoka kwa waandishi wa habari mkoani humo kutumia vyombo vyao kwa kutoa elimu kwa umma kupitia vipindi mbalimbali, kueleza madhara ya kuchagua viongozi kwa misingi ya kupeana rushwa.

Kwa upande wake, Kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa Kigoma, Jacob Ruvilo amesema, waandishi wa habari wako tayari kufanya kazi na TAKUKURU na kwamba wameomba taasisi hiyo kutoa ushirikiano, hasa taarifa za matukio ya wagombea  wanaokamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Mwisho.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi