Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2025

MKURUGENZI WA BODI YA CHAI TANZANIA(TTB) BEATRICE BANZI, AMEISHUKURU SER...

Picha

TAKUKURU YAWATEGA WALAJI, WATOA RUSHWA UCHAGUZI MKUU

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kigoma imesema kuwa   ina vyanzo vipya vya kupata taarifa na mbinu za kisasa, itakazozitumia kudhibiti vitendo vya rushwa katika hatua mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu katika mwaka huu. Hayo yamesemwa na Ofisa Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU Mkoa Kigoma, Abecha Bakari katika kikao kazi na waandishi wa Habari, kuweka mkakati wa pamoja wa ushirikiano katika kufanya kazi wakati wa Uchaguzi Mkuu. “Pamoja na mambo mengine, pia tumeongeza vyanzo vya taarifa na namna ya kupata taarifa hizo, lakini pia na namna ya   kuzifanyia kazi, hivyo tuna uhakika kuwa mwaka huu udhibiti wa vitendo vya utoaji na upokeaji rushwa utadhibitiwa,” amesema Bakari. Naye Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa Kigoma, John Mgallah aliomba ushirikiano kutoka kwa waandishi wa habari mkoani humo kutumia vyombo vyao kwa kutoa elimu kwa umma kupitia vipindi mbalimbali, kueleza madhara ya kuchagua viongozi kwa misingi ya ...

Wafanyakazi wa majumbani wamwangukia Rais Samia -

Picha
-Wamwomba aridhie Mkataba wa ILO kuwaokoa taabuni Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassa, imeombwa kukamilisha mchakato wa kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) namba 189 na kupitisha ili kuwezesha haki za msingi za wafanyakazi wa majumbani. Rais Samia Suluhu Hassan Ombi hilo limetolewa na wafanyakazi wa majumbani, wakieleza kuwa mkataba huo wa kazi zenye staha utawasaidia kupata haki na kuheshimiwa kama wafanyakazi wa sekta nyingine. Wametoa ombi hilo walipokuwa wakizungumza katika Kikao Kazi kilichowakutanisha kwa siku mbili mjini Morogoro, ambapo wamepata Mafunzo ya Utatuzi wa Migogoro ya Wafanyakazi wa Majumbani. Mwenyekiti wa Wafanyakazi wa Majumbani Tanzania, Zanini Athuman anasema mkataba huo wa ILO unaweka wazi stahiki halali kwa wafanyakazi wa majumbani, ikiwemo kupewa mapumziko ya kutosha, kuishi katika mazingira ya heshima (hasa kwa wanaoishi kwa waajiri). “Pamoja na uwepo wa sheria mbalimbali hapa...

Ni mapema mno kusahau mbunge wako aliyebwagwa CCM

Picha
  -CCM yawaambia wasikate tamaa, nafasi bado zipo nyingi  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutangaza majina ya wanachama wake waliopita katika mchujo, hatua za awali kwenda kwenye kura za maoni majimboni, ukiacha tabasamu kwa waliopitishwa na kilio kwa ambao hawakuteuliwa, sasa ni wazi chama hicho tawala kimewabwaga baadhi ya wanachama wake waliokuwa wabunge kwenye Bunge linalomaliza muda wake, wakiwamo wabunge maarufu. Hakika ni mapema mno kusahau mbunge wako aliyetia nia kuwania tena ubunge jina lake likakatwa, lakini ndivyo ilivyo kwani  J ulai 29,2025 Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla ametangaza majina    ya watakaopigiwa kura ili kupata wagombea ubunge wa majimbo 272,bil kuwepo majina ya wabunge takriban 27 wanaomaliza kipindi cha kuwa madarakani. Makalla ametaja wateule hao kutoka watia nia takriban 5,000 waliotia nia kuwania kuteuliwa na chama hicho tawala kuwania ubunge katika Uchaguzi ...

Wagombea udiwani wa kata yako Dar hawa hapa

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam kimeweka hadharani majina ya wanachama wake waliopita kwenye chekeche na kuteuliwa na vikao vya juu vya chama hicho kwenda kupigiwa kura za maoni kuwania nafasi za udiwani. Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu Tangazo hilo limejumuisha wagombea wa udiwani katika kata zote za mkoa huo wenye wilaya tano za Ilala, Kinondoni, Ubungo, Kigamboni na Temeke, huku ukiwa na majimbo 11 ya uchaguzi ambayo ni Kivule, Kigamboni, Ilala, Temeke, Ubungo, Kibamba, Kawe, Ukonga, Chamazi, Mbagala na Kinondoni. Mkoa wa dar es Salaam una takriban kata 102 ambazo mmoja wa watia nia hao wa CCM watakaopigiwa kura za maoni, atapata nafasi kukiwakilisha chama chake kuwania udiwani kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 29. Yafuatayo ni majina ya Wilaya, Kata na majina ya walioteuliwa kupigiwa kura za maoni; CHAMA CHA MAPINDUZI   MKOA WA DAR ES SALAAM  WANACHAMA WALIOTEULIWA KUPIGIWA KURA ZA MAONI...