Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2025

Maswi aipongeza Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali

Picha
Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali imepongezwa kwa kuendelea kusimamia kwa weledi mashauri ya madai na usuluhishi hatua ambayo imesaidia Serikali kuongeza kasi katika kuwaletea wananchi maendeleo. Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakimu Maswi akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Mashauri na Uthibiti Ubora wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Mercy Kyamba alipotembelea banda la Ofisi hiyo wakati wa Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakim Maswi alipotembelea banda la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya 49 ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam. Maswi alisema kuwa uwepo wa weledi na ufanisi katika uendeshaji wa mashauri ya madai, usuluhishi, Katiba, Haki za Binadamu na Uchaguzi katika Ofisi hiyo umeongeza kasi katika kupunguza na kutatua migogoro ya kisheria kwa njia ya majadil...

REA yajidhatiti kufikisha lengo kitaifa nishati safi ya kupikia

Picha
-Mkurugenzi Mkuu REA abainisha hatua zinazochukuliwa -Amshukuru Rais Samia kwa kuwezesha Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia. Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy, (kushoto),akipata maelezo kuhusu bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia zinazosambazwa na Kampuni ya Jucho Chanya kutoka kwa Ofisa Masoko wa kampuni hiyo, Ibrahim Kikoti katika Banda la REA kwenye Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa jijiniDar es SalaamJulai 7, 2025 Amebainisha hayo Julai 07, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA). “REA inalo jukumu la kuhakikisha maeneo yote ya vijijini yanapata aina zote za nishati s...