-Mambo yote Dar sasa Morocco Square
-Kuingiza Shilingi Bilioni 9 kwa mwaka
Mwandishi
Wetu, daimatznews@gmail.com
Morocco Square, moja ya miradi ya kifahari na kipekee nchini Tanzania uliotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), sasa umekamilika ukiwa ndio alama mpya ya maisha ya kisasa jijini Dar es Salaam.
![]() |
Sehemu ya jengo la kisasa Morocco Sqare linavyoonekana |
Alama
hiyo kubwa ya aina yake, imejengwa katika makutano ya Barabara za Mwai Kibaki,
Ali Hassan Mwinyi na Ursino eneo la Regent Estate, wilayani Kinondoni, umezingatia mambo yote muhimu
yanayohitajika kwa maisha ya mwanadamu anayeishi kisasa.
Kupitia
mradi huo wa kipekee, NHC imejenga majengo manne kwenye msingi mmoja, jengo moja likiwa ni hoteli, la pili ofisi
mbalimbali, jengo la tatu ni la biashara na la nne ni makaziya watu.
Huu ni ukweli halisi wa mradi huo uliozinduliwa Novemba 23 mwaka huu kwani unapotembelea eneo hilo utashuhudia maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya matumizi ya kibiashara, makazi na burudani. Vyote vikiwa katika eneo moja, hivyo kuvutia wawekezaji na wakazi wa jiji hilo kufika hapo, kufanya manunuzi, hata kufurahia maisha. Unaweza kusema mambo yote Dar sasa Morocco Square.
Jengo hilo linalojulikana kwa jina la Morocco Square lililojengwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 137 ni alama mpya ya kazi nzuri zilizofanywa na NHC Dar es Salaam na Tanzania nzima linalobeba nyumba za makazi, ofisi, maeneo ya biashara na burudani yakiwa kwenye msingi wa jengo moja.
Hakuna wa kubisha kwamba Morocco Square ni
ishara ya maendeleo ya kisasa nchini, ikiwa ni mradi wa matumizi mchanganyiko
unaojumuisha majengo manne makubwa: mawili kwa ajili ya ofisi, moja kwa ajili
ya makazi na lingine kwa ajili ya hoteli.
Majengo
haya yameundwa kwa viwango vya juu ili kutoa nafasi bora za kibiashara na
makazi yenye huduma za hali ya juu na kisasa zaidi.
Morocco
Square inajivunia majengo mawili ya ofisi yenye ghorofa 22 na 19, yanayojumuisha
maduka kwenye ghorofa za chini hadi ya pili, huku nafasi za ofisi zikianzia ghorofa ya tatu na kuendelea.
Majengo
hayo yanatoa mandhari ya kuvutia yanayofaa
kwa kampuni kubwa, biashara za kitaifa na kimataifa, pia kampuni zenye kuhitaji
mazingira ya kazi ya kisasa na yenye miundombinu yenye ubora wa hali ya juu.
Pia
kuna jengo la maduka lenye ngazi tatu, likichukua mita za mraba 28,873, likiwa
na maduka mbalimbali ya vyakula, mavazi, mitindo, na maeneo ya burudani.
Ndani
ya Morocco Square wateja wanaweza kufurahia sinema, vyumba vya michezo kwa
watoto na huduma mbalimbali zinazoongeza mvuto wa mradi huo kwa familia na watu
wa rika zote.
Kwa
upande wa makazi, Morocco Square inatoa fusra tofauti za kuchagua zinazokidhi
mahitaji ya makazi ya kisasa katika mradi unaojumuisha vyumba vya kulala vitatu
na vinne, duplex na vyumba vya kifahari vya ghorofa ambavyo vinafaa kwa wakazi
wanaotafuta maisha ya hadhi ya juu na yenye faraja jijini.
Hoteli
na Huduma za ziada
Jengo
la hoteli lenye ghorofa 16 na vyumba 81 vya studio linawapa wageni wa muda
mfupi na mrefu mahali pa kupumzika panapotoa burudani na starehe kamili. Hoteli
hii inayoendeshwa na kampuni ya Kihindi inatoa huduma zinazokidhi viwango vya
kimataifa, huku ikichangia katika kukuza sekta ya utalii na biashara jijini Dar
es Salaam.
Morocco
Square pia imejengwa kwa ajili ya huduma za kisasa zaidi, ikiwemo nafasi za
maegesho zinazochukua magari zaidi ya 2,000, eneo la kutua helikopta, bwawa la
kuogelea, klabu ya burudani, maduka ya kahawa, likiwa pia na jenereta za
dharura na mfumo wa usalama wa hali ya juu. Hizo zote ni huduma zinazofanya
eneohilo kuwa na mazingira bora na salama kwa wapangaji na wateja.
Uwekezaji
wenye faida kwa wawekezaji
Kwa Shirika la Nyumba la Taifa ( NHC), mradi huu ni zaidi ya jengo, ni uwekezaji mkubwa utakaozalisha wastani wa mapato yanayofikia Shilingi milioni 850 kila mwezi kila mwezi kutoka kwa wapangaji, hivyo kufikisha takribani Shilingi bilioni 9 kwa mwaka.
![]() |
Mwonekano wa nje wa Moocco Square |
Mapato
hayo ni sehemu ya mkakati wa NHC wa kuhakikisha Serikali inarejesha fedha zake
kupitia mapato yanayotokana na mradi huu.
Morocco
Square pia inatoa fursa za kipekee kwa wawekezaji kutokana na kuwa eneo lake la
kipekee katikati ya jiji, pia ukaribu wake na huduma muhimu za kijamii.
Eneo
hilo linavutia wateja wa viwango vyote, wakiwemo wafanyabiashara, familia, hata
watalii kutokana na mazingira bora ya biashara, makazi na burudani.
Kwa
NHC, kukamilika kwa Morocco Square ni kielelezo cha mafanikio ya utekelezaji wa
sera za Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, zinazolenga
kuongeza thamani ya mali na kutoa huduma bora kwa Watanzania. Morocco Square
inatoa mwaliko kwa wakazi na wageni kufika eneo hilo ili kufurahia mazingira ya kisasa na fursa tele
zinazopatikana hapo.
0 Maoni