Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2026

MAELEKEZO YA RAIS DK. SAMIA MRADI UJENZI MATENKI YA MAFUTA HAYA HAPA

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amezipa maelekezo maalum wizara na taasisi za Serikali akizitaka kuhakikisha Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam unatekelezwa kwa wakati na kukidhi viwango vya kimataifa. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, Machi 3, 2026. Ameiagiza pia Wizara ya Nishati, kuhakikisha inaimarisha miundombinu ya hifadhi ya mafuta na taifa linakuwa na akiba ya kutosha, ili kukabiliana na misukosuko ya bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia, huku akieleza kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani ni changamoto inayoongeza umuhimu wa kuwa na miundombinu madhubuti ya nishati. Rais Dk. Samia ametoa maelekezo hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati, Machi 3, 2026, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kwamba uwekezaji huo ni ha...

TAWA KANDA MAALUM DAR YAHIMIZA UHIFADHI WALIO HATARINI KUTOWEKA

Picha
-Yaadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani -Yaita wananchi kujionea vivutio vya mjini  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Uhifadhi Wanyamapori nchini (TAWA), Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo Machi 3, 2026, imeungana na wadau wengine wa sekta hiyo katika kuadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani, inayoadhimishwa Machi 3 kila mwaka, ikihimiza jamii kushiriki katika kulinda wanyama walio katika hatari ya kutoweka   kwa faida ya taifa leo na vizazi vijavyo. Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy  Kamanda wa Uhifadhi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy ametoa wito huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Machi 3, 2026   alipokuwa akizungumzia maadhimisho hayo yaliyobeba Kauli mbiu isemayo; ‘Mimea dawa, manukato, uhifadhi urithi na kuboresha maisha.’ Amesema kauli mbiu hiyo inahamasisha wananchi kutunza hifadhi wanyama pori na mimea, lakini pia TAWA imetumia siku hiyo kuwapa elimu na kuwahamasisha wananchi k...