Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2024

*NHC Yapata Tuzo ya Uandaaji Bora wa Hesabu kwa Mashirika ya Umma ya kibishara

https://www.instagram.com/p/DC96pM4sLVu/?igsh=YzljYTk1ODg3Zg== Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeendelea kuonyesha ubora wake katika usimamizi wa fedha baada ya kutunukiwa tuzo ya mshindi wa tatu wa Uandaaji Bora wa  Hesabu kwa Mashirika ya Umma kwa kufuata viwango vya kimataifa vya uandaaji wa hesabu (International Financial Reporting Standards - IFRS).  Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika la Nyumba la Taiafa(NHC), CPA Adolph Kasegenya na Mgeni Rasmi CPA, Benjamin Mashauri kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha katika hafla iliyofanyika leo kwenye Kituo cha Wahasibu kilichopo Bunju, Jijini Dar es Salaam. Katika hafla hiyo, Bw. Mashauri aliwapongeza Washindi wote likiwamo Shirika la Nyumba la Taifa kwa uwazi, uwajibikaji na umahiri wake katika kuandaa taarifa za kifedha zinazokidhi viwango vya kimataifa.  Alibainisha kuwa tuzo hiyo ni kielelezo cha juhudi za Shirika hilo katika kuboresha usimamizi wa fedha, uwazi wa taarifa na uwajibikaji, ha...

Rais Dk. Samia kufungua kongamano STICE2024

Picha
 Kuzindua Mfuko Mikopo Nafuu  Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Rais Dk, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi na kufungua Kongamano na Maonesho ya Tisa ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu  (STICE2024 ), ambapo pia atazindua Mfuko wa Mikopo Nafuu na kutoa fedha kwa watafiti. Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dk, Amos Nungu Akizungumza katika kikao kazi na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dk. Amos Muhunda Nungu amesema Rais atafungua kongamano hilo Desemba 2, 2024 ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini humo. “Tutaanza na Shilingi Bilioni 2.3 za kuwakopesha watafiti waliokidhi vigezo kutokana na maandikowaliyoleta COSTECH, Rais atazindua mfuko huo. Fedha hizo ni kwa kuanzia, tutaendelea kupata fedha kwa wadau na Serikali,” amesema Dk Amos na kufafanua; “Kauli mbiu ya Kongamano kwa mwaka huu ni; Matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu katika Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi ...

NHC yataja mikakati tatu ya kuimarisha sekta ya nyumba nchini

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeibua mikakati mitatu muhimu ambayo ikitekelezwa itasaidia kuinua sekta ya nyumba nchini na kuwezesha Watanzania kumiliki nyumba bora kwa urahisi.  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah (kushoto), akiongozana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya  Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC) Vuma Augustinona wajumbe wa kamati hiyo kutembelea miradi ya ujenzi ofisi za Wizara Nane za Serikali, eneo la Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma, Oktoba 26, 2024. Mikakati hiyo ni pamoja na kuanzisha sera ya unafuu wa kodi kwenye vifaa vya ujenzi, kuunda mfuko maalum wa miundombinu ya huduma muhimu, na kupunguza riba kwenye mikopo ya sekta ndogo ya nyumba. Akiwasilisha mapendekezo haya mbele ya Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC) jijini Dodoma tarehe 26 Oktoba, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, alisema kuwa utekelezaji wa hatua hizi utachochea ukuaji wa sekta ya nyumba nc...

TEF 'walia' na Waziri Silaa

Picha
Exuperius Kachenje Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limeeleza kutoridhishwa kwake na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa kushindwa kufika kwenye matukio ya wadau wa habari ikiwemo kufungua Mkutano Mkuu wa Nane wa jukwaa hilo unaofanyika Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile (Aliyesimama) akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Nane wa Jukwaa hilo unaofanyika Novemba 6 hadi 9, 2024 jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wa Novemba 6 hadi 9, 2024, Waziri Silaa amewakilishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Nicholaus Mkapa. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile alipokuwa akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo leo Novemba 7, 2024 katika ukumbi wa NSSF Mafao House, Ilala Dar es Salaam,uliobeba kauli mbiu; "Weledi kwa Uhimilivu wa Vyombo vya Habari." "Sisi Wahariri hatufurahishwi na hatuwezi kuficha jambo hili, hatufurahishwi na Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknoloji...